Tuesday, November 6, 2018

TAIFA STARS YATUA SALAMA SOUTH AFRIKA KWA KAMBI YA WIKI 2

Taifa stars

Kikosi cha Stars kimewasili salama huko Afrika Kusini kwa kambi maalum kujiandaa na mechi dhidi ya Lesotho kuwania kufuzu AFCON 2019.


Wachezaji waliosafiri na timu ni makipa Aishi Manula (Simba SC), Aaron Kalambo (Tz Prisons) Beno Kakolanya (Yanga SC) na Benedictor Tinocco (Mtibwa Sugar)

Mabeki ni Shomary Kapombe (Simba), Salum Kimenya (Tz Prisons) Erasto Nyoni (Simba) Ally ‘Sonso’ Abdulkarim (Lipuli) Kelvin Yondani (Yanga), Gardiel Michael (Yanga), Aggrey Morris (Azam) na Abdallah Kheri (Azam)

-Viungo ni Salum Abubakar ‘Sure Boy’ (Azam) Mudathir Yahya (Azam) Feisal Salum Fei Toto (Yanga), Jonas Mkude (Simba), Shiza Kichuya (Simba). Washambuliaji ni Thomas Ulimwengu (Huru), John Bocco (Simba) na Yahya Zayd (Azam)

Aidha wachezaji wanaokipiga nje ya Tanzania wataungana na wenzao mbele ya safari tayari kwa mechi hiyo itakayopigwa Novemba 18.

Saturday, April 23, 2016

KITAMBI AIOMBEA MABAYA YANGA KOMBE LA FA

IMG_0055
Kocha msaidizi wa Azam FC Denis Kitambi amesema nguvu zao zote wanazihamishia kwenye ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara pamoja na michuano ya kombe la Azam Sports Federation Cup (FA) kufuatia kushindwa kufanya vizuri kwenye mashindano ya Afrika.

Azam imerejea jana ikitokea Tunisia ilikotolewa kwenye kombe la shirikisho Afrika kwa kipigo cha magoli 3-0 dhidi ya Esperance.
“Sasahivi hakuna nafasi ya kufanya kosa lolote, hatuwezi kupoteza mechi yoyote kwasababu kupoteza mechi au kusuluhu maana yake ubingwa tumeuacha. Kwetu sisi ni kuhakikisha tunashinda michezo yetu na inawezekana Yanga wakapoteza pointi kwenye mechi zao za ugenini”.

“Mchezo wa FA Cup dhidi ya Mwadui ni muhimu sana kwasababu bingwa wa FA Cup ndiyo atapata nafasi ya kushiriki mashindano ya Afrika, kwahiyo kwetu sisi mchezo wetu dhidi ya Mwadui ni muhimu sana kwasababu ndiyo nafasi pekee ambayo bado ipo mkononi mwetu kuweza kushiriki michuano ya kimataifa”.

Jumapili April 24, Azam itacheza mchezo wa nusu fainali ya FC Cup dhidi ya Mwadui FC mchezo utakaofanyika kwenye uwanja wa Mwadui Complex, Shinyanga wakati huo Yanga itakuwa ikicheza dhidi ya Coastal Union jijini Tanga washindi wa mechi hizo watafuzu kucheza hatua ya fainali ya michuano hiyo ambapo bingwa ataiwakilisha nchi kwenye kombe la shirikisho msimu ujao.


Friday, April 22, 2016

YANGA YATUPWA HUKU KWENYE MICHUANO YA SHIRIKISHO AFRIKA CAF..


CAF-cover
Kufuatia kuondoshwa kwenye michuano ya klabu bingwa barani Afrika hatua ya 16 bora, klabu ya Yanga imeangukia kwenye michuano ya kombe la Shirikisho Afrika. Kwa mujibu wa kanuni za CAF, vilabu vyote vinavyotupwa nje ya mashindano ya klabu bingwa Afrika vinakutana na washindi wa hatua ya 16 bora ya kombe la shirikisho kukipiga mchezo wa playoff unaoamua timu gani inasonga mbele kwenye hatua ya makundi katika kombe la shirikisho.

Usiku wa Jumatano Yanga ilisukumwa nje ya kombe la mabingwa Afrika na klabu ya Al Ahly ya Misri kwa kufungwa magoli 2-1 ugenini hivyo kuenguliwa kwenye michuano hiyo kwa jumla ya magoli 3-2 baada timu hizo kutoka sare ya kufungana goli 1-1 kwenye mchezo wa kwanza uliochezwa Dar.

April 21 imechezeshwa droo ya kuamua ni timu gani zitakutana kwenye mechi za mchujo zitakazoamua ni timu gani zitafuzu hatua ya makundi ya kombe la shirikisho Afrika.

Mabingwa watetezi wa VPL Yanga wamepangwa kucheza na klabu ya Sagrada Esparanca ya Angola ambapo Yanga wataanzia nyumbani mchezo wa kwanza (uwanja wa taifa, Tanzania) kati ya May 6-8 huku mchezo wa marudiano ukipangwa kufanyika Angola kati ya May 17-18, 2016.

RATIBA KAMILI.
Yanga-Angola

FUATILIA UTABIRI WA MICHEZO MBALIMBALI PALE UINGEREZA NA PAUL MERSON.

Merson's predictions: Tottenham to narrow gap on leaders Leicester


Sky Sports' Paul Merson is back to look ahead to another crucial round of Premier League fixtures.
Eight points off a maiden top-flight crown, Leicester, without the suspended Jamie Vardy, host Swansea on Super Sunday as they look to stretch the gap between themselves and Tottenham.
Second-placed Spurs will be waiting, ready to pounce if the Foxes slip up when they entertain West Brom on Monday Night Football.

Before all of that, the race for survival takes centre stage as Sunderland look to move out of the relegation zone when they face Arsenal at the Stadium of Light in Sunday's early kick-off.
There is also the little matter of the FA Cup semi-finals, where Crystal Palace, Everton, Manchester United and Watford jostle for a place in the Wembley showpiece.
Read on to see who the Magic Man is backing...

Last week's predictions

Result Merse's prediction
Norwich 0-3 Sunderland 1-1
Everton 1-1 So'ton 2-2
Man Utd 1-0 Aston Villa 3-0
Newcastle 3-0 Swansea 2-1
West Brom 0-1 Watford 2-0
Chelsea 0-3 Man City 2-1
B'mouth 1-2 Liverpool 1-2
Leicester 2-2 West Ham 2-1
Arsenal 1-1 Palace 3-0
Stoke 0-4 Spurs 0-4
Leicester v Swansea - Super Sunday, 4.15pm

This game was a gimme for Leicester last week, now Jamie Vardy is suspended it's not. I don't think Vardy is a great player but without him how are Leicester going to open up the game? He stretches defences and creates space for midfielders on the ball and I can't see who will be able to replace that pace.
I just don't see Leicester winning without Vardy, he is a massive, massive miss. Swansea will just play around halfway, suffocate the Foxes and come away with a point which will blow the title race wide open.

Leicester vs Swansea

April 24, 2016, 4:00pm
Live on
PAUL PREDICTS: 1-1 (Sky Bet odds 5/1)
Tottenham v West Brom - Monday Night Football, 8pm

Fair play to West Brom, they got their 40 points on the board early doors ahead of an atrocious final run of fixtures. It starts with Spurs, who were outstanding at Stoke. It doesn't even pain me to see Spurs where they are at the moment, they are a very good team. Hopefully their success kicks Arsenal into gear. If this Tottenham team stays together and they get a couple more players they'll be favourites for the title next season.

Tottenham vs W Brom

April 25, 2016, 7:00pm
Live on
PAUL PREDICTS: 3-0 (Sky Bet odds 11/2)
Sunderland v Arsenal - Super Sunday, 2.05pm

I watched Arsenal on Sunday and it was one of the flattest performances I've seen, they just went through the motions. It was so quiet at the Emirates that I heard Petr Cech shout 'keeper' when clearing a ball. How is that possible in front of 60,000 people? Arsenal beat West Brom on Thursday, but they should have beaten Palace too. Sunderland, meanwhile, have picked up under Big Sam, winning at Norwich last week. I fancy them to edge closer to safety with a point, but they do need to score first.

S'land vs Arsenal

April 24, 2016, 1:00pm
Live on
PAUL PREDICTS: 1-1 (Sky Bet odds 11/2)
Man City v Stoke - Saturday, 12.45pm

The problem with Man City is that you don't know which team is going to turn up. Will it be the one that won 3-0 at Chelsea or will it be the team that came off the pitch lucky to have earned a 1-1 draw with Newcastle? Stoke are on holiday and you cannot play football with flip-flops on! They've done their hard work, though, they're safe and you can understand that, particularly when a few players will be at the Euros. I suspect Sergio Aguero will be rested as City will have one eye on the Champions League semi-final with Real Madrid, but I still expect them to win.
PAUL PREDICTS: 2-0 (Sky Bet odds 5/1)
Aston Villa v Southampton - Saturday, 3pm

What score do you want? I can't see anything other than a Southampton win. I felt sorry for Joleon Lescott in the week because his comments about relegation being a relief were not meant like that. He meant the club could concentrate on bouncing back next season, so a lot of the criticism he received was unwarranted. Villa should give the kids a chance and see what they're like ahead of next season - see who can be kept and who can't.
PAUL PREDICTS: 0-2 (Sky Bet odds 5/1)
Bournemouth v Chelsea - Saturday, 3pm

This is a hard game. Chelsea could have conceded six against Man City on Saturday, their season is over, they've got players going to the Euros and they can't win a game. I'm not sure which way the game will go but I expect a game full of goals, with Bournemouth needing to bounce back from their defeat to Liverpool.
PAUL PREDICTS: 2-2 (Sky Bet odds 12/1)
Liverpool v Newcastle - Saturday, 3pm

I was impressed with Newcastle against Man City, they were good. Liverpool keep on getting better and better under Jurgen Klopp and they put Everton to the sword in the derby. I fancy Liverpool here but, with a Europa League semi-final with Villarreal coming up, they may rest players - that said they still turn in decent performances when they do change their team. This is where luck in the relegation fight comes in because if Liverpool were challenging for the top four they would play a full-strength side, and that may help Newcastle's cause. I expect Liverpool to just earn the win but I wouldn't be surprised if it's a draw.
PAUL PREDICTS: 2-1 (Sky Bet odds 7/1)

Midweek predictions

Result Merse's prediction
Newcastle 1-1 Man City 0-2
Liverpool 4-0 Everton 3-0
Arsenal ?-? West Brom 3-0
FA Cup semi-finals
Everton v Man Utd - Saturday, 5.15pm

I don't see how Roberto Martinez can last if he loses at Wembley. He has got things horribly wrong this week. He should have played his strongest team and won against Southampton and then told fans he had to rest everyone against Liverpool in preparation for the semi-final. Instead he rested everyone against Southampton and got booed off and then played his best team against Liverpool and got battered. For the first time he looked lost on the sidelines, the fans have turned and I don't see how he can hold on if they lose. I felt sorry for him but it's a situation of his own making, this is a good team that is nowhere.

United will win at Wembley, I can't see Everton stopping them. Marcus Rashford is some player and his goal against Villa was as good as it gets - he'll be a top-drawer player. Three months ago you would have backed Everton to win this game all day long, not now.
PAUL PREDICTS: 1-2 (Sky Bet odds 15/2)
Crystal Palace v Watford - Sunday, 4pm

I fancy Palace here, they've just got the edge over Watford. Deeney, who missed a penalty at West Ham, and Ighalo have gone quiet recently and confidence at the club can't be great. When the game starts to open up Palace have got more match winners for and I expect them to just edge a tight contest.
PAUL PREDICTS: 1-0 (Sky Bet odds 6/1)

MCHEZAJI WA ZAMANI WA SIMBA ATOA YA MOYONI.......

Mlinzi wa zamani wa timu ya Simba SC na timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars,) Lubigisa Madata Lubigisa amesema kinachoendelea katika klabu yake hiyo ya zamani ni ‘matokeo ya ubinafsi na kutowajibika ipasavyo’ kwa uongozi wa juu ambao kwa mawazo yake (Lubigisa) wameshindwa kuwa karibu na wachezaji na kutowatimizia mahitaji yao muhimu.

Madata ambaye alikuwa sehemu ya kikosi cha timu hiyo kilichofuzu kwa hatua ya makundi ya ligi ya mabingwa Afrika mwaka 2003 amesema hayo wakati nilipomuomba mtazamo wake kuhusu mwenendo wa timu hiyo inayosotea taji la ligi kuu kwa msimu wa nne mfululizo hivi sasa.

“Kinacho endelea Simba sasahivi ni maslahi binafsi ya viongozi. Viongozi wanajali sana maslahi yao binafsi na kusahau kama jukumu lao la kuifanya Simba ishinde, kiongozi aliye makini tena wa club kubwa kama Simba anaye hitaji matokeo mazuri ili aongoze ligi hawezi kukubali kufungwa na Toto.”

“Ninachokiona kwa uongozi ni hawataki kutumia pesa ili washinde mechi kama ile, kiongozi lazima uwe karibu na wachezaji wako tumia pesa kwa wachezaji wako waahidi pesa ili wacheze kwa moyo na kujituma zaidi.”

Saturday, June 6, 2015


DE GEA AWAAGHA WENZAKE MAN UNITED

KWAHERI: David De Gea awaaga wenzake Old Trafford


MIKONO ya kipa, David de Gea, iliyotumika kuibeba Man United katika msimu uliomalizika hivi karibuni, inadaiwa kuwa imetumika pia kuwaaga wachezaji wenzake kikosini humo hivi karibuni katika uwanja wa mazoezi wa timu hiyo, Carrington.
Inadaiwa kipa huyo hataivaa tena jezi ya Man United na ripoti za England zinadai ameshawaaga wachezaji wenzake, benchi la ufundi na wafanyakazi wa klabu.
Staa huyo aliyenunuliwa kwa Pauni 18 milioni Juni 2011 na kuwa kipa ghali England, amegoma kusaini mkataba mpya Old Trafford ambao ungemfanya awe analipwa Pauni 200,000 kwa wiki.
Rais wa Real Madrid, Florentino Perez anaamini atampata De Gea kwa Pauni 25 milioni tu kwa kuwa mkataba wake Old Trafford umebakiza miezi 14 na kipa huyo mzaliwa wa Madrid, amedhamiria kurudi katika jiji hilo ambalo ni makazi ya mpenzi wake, Edurne Garcia Almagro, staa wa muziki wa Pop.
Madrid ilikuwa inasubiri imalize suala lake la kuachana na kocha, Carlo Ancelotti, kabla ya kumgeukia De Gea ambaye atakuwa mbadala wa muda mrefu wa kipa wao, Iker Casillas, ambaye nyakati zinaonekana kumpita.
Kocha wa Man United, Louis van Gaal, ambaye yupo likizoni Ureno, amekiri hana ubavu wa kumzuia kipa huyo asiondoke kurudi kwao Hispania.
“Sidhani kama ninaweza kumshawishi abaki kwani anajua kila kitu ilichonacho Man United. Sihitaji kusema lolote, yeye mwenyewe anahisi kila kitu. Umewaona mashabiki (wanavyompenda) inashangaza sana. Atakapoondoka, atapoteza hilo. Ana sifa nyingi. Inabidi aamue mwenyewe,” alisema Van Gaal.
Licha ya kubembelezwa kiaina na Van Gaal, De Gea ametoa kauli inayoashiria kwamba ataondoka baada ya kutotaka kuzungumzia hali yake ya baadaye huku akisisitiza yuko likizo kwa sasa.

ZIJUE A,K,A ZA WACHEZAJI TOFAUTI WA BONGO WAKIJIFANANISHA NA WA NCHI ZA NJE .. SWALI LA KUJIULIZA JE KWELI WANAENDANA?

Unawajua Cannavaro, Boban, Nemanja Vidic, Garincha, Fabregas, Barthez wa Bongo? Wasome hapa
SOKA la Tanzania limekuwa likipiga hatua siku hadi siku na hiyo inatokana na kuibuka kwa vipija vingi vya vijana ambao wanavutiwa na mchezo huo unaoongoza kuwa na mashabiki wengi duniani.
Utaditi uliofanywa na Goal unaonyesha asilimia 65 ya vijana wa kiume wa Tanzania wanapenda mchezo wa soka na wengi wao wamejiingiza kwenye mchezo huo kama siyo kwa kuucheza basi kwa kushangilia timu mbalimba iwe za ndani au za Barani Ulaya.

Kutokana na soka kuwa mchezo maarufu kupita yote duniani na ukiongeza na utandawazi uliopo kupitia Televisheni hata wachezaji wakubwa wanaocheza timu zinazo shiriki ligi kuu ya Vodacom wamekuwa ni wafuatiliaji wa zuri wa ligi za Ulaya na wengine kutokana na uhodari wame wamepachikwa majina ya utani ya wachezaji wa Ulaya na mashabiki wao na wengine wamejipa wao wenyewe.
Hapa chini Mtandao wa Goal unakuletea wachezaji nane wenye umaarufu mkubwa katika Ligi Kuu ya Vodacom kwa kutumia AKA za majina ya wachezaji wa Ulaya kiasi cha majina yao halisi kutofahamika kwa mashabiki.

1.Nadir Haroub ‘Cannavaro huyu ni nahodha wa klabu kubwa Tanzania inayoongoza ligi kuu ya Vodacom na pia ni nahodha wa timu ya taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’ kutokana na nafasi anayocheza uwanjani na mchango wake kwa timu hizo mbili amebatizwa jina la nahodha wa timu ya taifa ya Italia Fabio Cannavaro.
Mchango wa Hadir Haroub kwa timu hizi mbili haupishani sana na Cannavaro halisi wa Italia kwani amekuwa akicheza kwa bidii ya hali ya juu na wakati mwingine ameweza kuifungia timu yake mabao mahimu katika mechi muhimu na pindi anapokosekana labda kwa matatizo ya majeruhi ama kutumikia adhabu basi hali huwa tete na hofu huongezeka kwa mashabiki wake.

2.Haruna Moshi ‘Boban’ huyu ni kiungo mshambuliaji wa timu ya Friends Rangars zamani aliwahi kutamba na klabu kubwa ya Simba na hata Coastal Union alipewa jina la Boban na mashabiki wa SImba kutokana na uwezo wake anapokuwa dimbani ambao ulikuwa ukifanana na ule wa Mcroatia Zvonimir Boban aliyetamba na klabu ya AC Milani ya Italia.

Mbali ya uwezo wake awapo dimbani lakini Boban wa Tanzania amekuwa na vituko vingi ambavyo vinamfanya awe mchezaji wakipee nchini na haikushangaza Agosti 2010 alipovunja mkataba na timu ya Gavle IF, ya Sweden aliyokuwa anaichezea kama Profeshino.

3.Kelvin Yondani , ‘Nemanja Vidic’ Huyu ni beki mwingine mwenye jina kubwa kwenye ligi ya Tanzania bara akiichezea Yanga na timu ya taifa ‘Taifa Stars’ uwezo wake wa kuwadhibiti washambuliaji hatari mashabiki wake wakati huo akiichezea Simba walimpa jina hilo wakimfananisha na Vidic ambaye kwa sasa anaichezea klabu ya Inter Millan ya Italia akitokea Mancherster United.
Sifa kubwa aliyokuwa nayo Yondan na kusababisha mashabiki hao kumfananisha na Vidic ni jitihada zake anazozifanya uwanjani za kulinda lango lake huku akiruka vichwa kwa kufunga au kuokoa kama ilivyo kwa mwenye jina hilo Mserbia Nemanja Vidic .

4.Steven Mapunda ‘Garincha’ Huyu ni winga wa zamani aliyewahi kutamba na klabu ya Simba na kidogo timu ya taifa ‘Taifa Stars kutokana na uwezo aliokuwa nao wa kupiga chenga akiwa kwenye kasi mashabiki wa soka walimbatiza jina la Garincha akifanianishwa na Mbrazili Manuel Francisco dos Santos
Uwezo wa mchezaji huyo aliyetamba na timu ya Brazili ulikuwa ni hatari kwa mabeki wa timu pinzani sawa na Mapunda ambaye kwa sasa ameshastaafu soka na yupo kwao Songea anaendeleza kipaji chake kwa kuibua vipaji vya soka.

5.Haruna Niyonzima ‘Fabregas’ Kiungo fundi raia wa Rwanda anayecheza soka la profeshino kwenye klabu ya Yanga ya Tanzania ni mmoja ya wachezaji maarufu Afrika Mashariki na Kati na kiwango chake cha kuichezesha timu na kutoa pasi za mabao kumewafanya mashabiki wa soka wa Rwanda kumpachika jina la kiungo huyo anayeichezea klabu ya Chalsea ya Uingereza kwa sasa.
Uwezo wa Niyonzima mbaye ni nahodha wa timu ya taifa ya Rwanda ‘Amavubi’ umeweza kuwavutia makocha wengi ambao wamekuwa wakimuhitaji kwa ajili ya kuzitumikia timu zao na huenda mwishoni mwa msimu huu kiungo huyo akaachana na Yanga na kurudi kwao Rwanda kuichezea APR kwani amegoma kuongeza kusaini mkataba mpya.

6.Wazir Mahadhi ‘Mendieta’ Huyu ni kiungo wazamani wa Tanzania aliyepata umaarufu mkubwa wakati akiichezea klabu ya Yanga kutokana na uwezo wake mashabiki wa soka waliamua kumpa jina la kiungo wa Hispania Gaizka Mendieta ambaye kwa sasa amestaafu soka .
Mara ya mwisho Wazir Mahadhi kuchezea timu za ligi kuu ya Vodacom ilikuwa ni msimu wa 2009/2010, wakati aliposajiliwa na Moro United na kuonyesha uwezo mkubwa pamoja na ukongwe aliokuwa nao lakini pamoja na mchango mkubwa timu hiyo ilishuka daraja mwishoni mwa msimu na yeye kuamua kustaafu rasmi kucheza soka.

7.Ally Mustaph ‘Barthez’ Huyu ni kipa changuo la kwanza kwa sasa kwenye klabu ya Yanga ambaye uwezo wake wakati huo akiichezea Ashanti ya Ilala 2006 ulisababisha mashabiki wa timu hiyo kumpachika jina la Fabian Barthez kipa wa Ufaransa na klabu ya Manchester United aliyefanya vizuri kwenye fainali za kombe la Dunia za mwaka 1998.
Jina la Barthez limemsaidia sana kipa huyo wa Tanzania kudumu kwenye soka kutokana na kupitia kwenye vipindi vigumu ikiwemo kukaa benchi kwa msimu mzima wakati alipohamia Simba huku kipa namba moja wakati huo akiwa Juma Kaseja, lakini uvumilivu wake ulikwisha baada ya kuhamia Yanga misimu mitatu mitatu iliyopita na kuipa ubingwa Yanga katika msimu wa kwanza lakini napo alipata matatizo baada ya kufungwa mabao matatu dhidi ya timu yake ya zamani Simba na kuwekwa benchi kwa muda mrefu kabla ya kupambana na kurudi kwenye nafasi yake.

8.Deogratius Munish ‘Dida’ Kama ilivyo kwa Batherz Munish naye ni mmoja wa makipa hodari anayeichezea klabu ya Yanga na timu ya taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’ uwezo wake akiwa na klabu za Simba, Mtibwa Sugar, Azam FC na sasa Yanga pamoja na urefu wake mashabiki walimpachika jina la DIDA wakimfananisha na kipa wa Brazili Nélson de Jesus da Silva aliyepata umaarufu mkubwa akiwa na klabu ya AC Millan ya Italia.
Ingawa Dida wa Brazili kwa sasa hana jina baada ya kurudi kucheza ligi ya kwao katika timu ya Sport Club Internacional lakini Dida wa Yanga bado yupo kwenye kiwango licha ya kukosa namba kwenye kikosi cha kwanza na hiyo ilitokana na uzembe alioufanya kwenye baadhi ya mechi na kocha Hans van der Pluijm kumpa nafasi Barthez.
Utumiaji wa majina hayo kumekuwa kukiongeza hamasa kubwa kwenye mechi za Ligi Kuu kwa sababu wachezaji hao wanalazimika kujituma zaidi kuonyesha tofauti na wengine kutokana na kufahamika zaidi na wakati mwingine kulinda heshima ya majina wanayoyatumia kwa kuonekana wapo juu kila siku.

NNI HATIMA YA DI MARIA NDANI YA MANCHESTER UNITED? FUATILIA MWENYEWE ALIVYOSEMA JANA KWENYE VYOMBO VYA HABARI

Angel Di Maria amekanusha tetesi zinazoeleza kuwa yupo katika mpango wa kutimka Manchester United na amesisitiza kuwa atarudi Old Trafford msimu ujao.

Nyota huyo wa kimataifa wa Argentina alijiunga na Man United kwa ada ya usajili ya paundi milioni 59.7 akitokea Real Madrid na kuvunja rekodi ya usajili nchini Uingereza, lakini ameshindwa kuonesha cheche katika msimu wake wa kwanza.

Di Maria ambaye yupo na timu ya taifa ya Argentina inayocheza michuano ya Copa America amesema hana mpango wa kuondoka Man United na anatarajia kurudisha kiwango chake msimu ujao chini ya Louis van Gaal.

“Nimemaliza msimu wangu wa kwanza kuichezea Manchester United,” Amewaambia The Sun. “Ulikuwa msimu mgumu kwangu. Nadhani ulikuwa mgumu kwasababu ilikuwa ni taifa lingine na klabu nyingine, ligi hii ni ngumu kuliko ya Hispania. Sikuweza kuendana nayo kwa haraka”.

Sasa nitacheza Copa America na kurudi kucheza Manchester United msimu wangu wa pili, nadhani nitarudi kwenye ubora wangu”.

Kiufupi tu ni kwamba Angel Di Maria amefanikiwa kuchukuwa tuzo baada ya goli lake alilofunga dhidi ya Liecester City kuchaguliwa kuwa gili bora la msimu baada ya kumpiku Chalie Adam na goli lake alilofunga dhidi ya chelsea kwa msimu uliopita wa ligi 2014-2015. .

KUMEKUCHAAA!!!! BARCELONA NA JUVENTUS WAKIWASILI UJERUMANI... WEKA KURA YAKO SASA NANI KUIBUKA NA USHINDI?


SAKATA LA MESSI NA SIMBA LAFIKIA PATAMU, TFF YATAKA KUKUTANA NAO





TFF imepokea kwa masikitiko makubwa taarifa za mgogoro wa kimkataba kati ya Mchezaji Ramadhani Singano wa klabu ya Simba.
TFF imeagiza mwakilishi wa klabu ya Simba pamoja na mchezaji wa Simba wafike ofisi za TFF siku ya Jumanne tarehe 09/06/2015 kwa mazungumzo. 
Kila upande umetakiwa uje na vielelezo vyake. 
Katika kipindi hiki cha kuelekea kwenye mazungumzo,TFF inaziasa pande zote mbili zijiepushe na kutoa matamko yanayoweza kuchochea hali ya kutoelewana na kuamsha hisia mbaya katika familia ya mpira wa Miguu Tanzania.
 IMETOLEWA NA SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)

Saturday, May 23, 2015

RATIBA MICHEZO YA MWISHO LIGI KUU ENGLAND - SEASON 2014-2015

Sunday 24 May 2015

IN CAT
 
Stoke CityvLiverpoolBritannia Stadium16:00
Newcastle UnitedvWest Ham UnitedSt. James' Park16:00
Manchester CityvSouthamptonEtihad Stadium16:00
Leicester CityvQueens Park RangersKing Power Stadium16:00
Hull CityvManchester UnitedThe KC Stadium16:00
EvertonvTottenham HotspurGoodison Park16:00
Crystal PalacevSwansea CitySelhurst Park16:00
ChelseavSunderlandStamford Bridge16:00
Aston VillavBurnleyVilla Park16:00
ArsenalvWest Bromwich AlbionEmirates Stadium16:00

NDEMLA, ISIHAKA HASSANI WAONGEZA MKATABA SIMBA






BEKI aliyewahi kuripotiwa kutakiwa na Real Madrid Castilla, inayoshiriki Ligi Daraja la Kwanza Hispania, maarufu kama Segunda B, Hassan Isihaka (pichani kulia) amesaini Mkataba mpya wa miaka mitatu na Simba SC.
Mapema mwaka huu, maskauti wa Real Madrid waliozuru Tanzania, walivutiwa na wachezaji wawili wa SImba SC, beki Isihaka Hassan na kiungo Ramadhani Singano ‘Messi’.

Timu hiyo ya pili ya mabingwa wa Ulaya, Real Madrid inayocheza mechi zake Uwanja wa Alfredo di Stefano, kupitia mwakilishi wake, Rayco Garcia iliwasilisha rasmi maombi yake kwa klabu ya Simba SC juu ya wachezaji hao.

Garcia alisema anawataka wawili hao Juni mwaka huu waende Hispania kufanyiwa majaribio katika timu hiyo na kama wakifuzu wataanza maisha mapya Ulaya.

Wakati bado Juni inabisha hodi, Isihaka anarefusha muda wa kuendelea kuitumikia Simba SC hadi mwaka 2018.

Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba SC, Zacharia Hans Poppe amesema  jana kwamba, mbali na Isihaka, kiungo chipukizi Said Hamisi Ndemla naye ameongeza Mkataba wa miaka mitatu pia.
“Chipukizi hawa wawili, wote wataendelea kufanya kazi Simba SC hadi mwaka 2018, na bado tunapitia ripoti ya benchi la Ufundi, ili kuboresha mikataba ya wachezaji wengine ambao tunahitaji kuendelea nao,”amesema Kapteni huyo wa zamani wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ).

FLANAGAN , IBE WASAINI KANDARASI MPYA NDANI YA LIVERPOOL

Wachezaji kinda wa Timu ya liverpool Jordan Ibe na Jonh Flanagan hatimae wamesaini mkataba mpya wa kuendelea kuitumikia klabu hiyo  hadi mwaka 2020.

TAIFA STARS HOVYOOOOOOOO

Timu ya taifa ya Tanzania Taifa Stars Jana ilipandishwa virago na kurejea Tanzania baada ya kupokea vichapo vitatu mfululizo kutoka kwa swazland,madagascar na lesotho.

Timu hiyo dhaifu kuwahi kutokea katika michuano hiyo aambayo walienda kushiriki kama waalikwa wakiwemo na timu ya taifa ya Ghana. Stars alioongozwa na Cap[tain wao John Bocco  baada ya kuchukua kitambaa hiko kutoka kwa Nadir Haroub amabaye ni majeruhi.

Mashabiki wa soka nchini Tanzania wanasema kwamba timu hiyo si ya taifa ni TFF kwani uteuzi wake ulifanywa kwa magumashi na kutoangalia uwezo wa mchezaji katika ligi iliyoisha hivi karibuni.

Kuna wachezaji wengi ambao wameonyesha kiwango kikubwa kama Salum Telela, Jonas Mkude, Hassani Kessy, Malimi Busungu, Rashidi Mandawa, David luhende  na wengineo wengi ambao wameonyesha kiwango kizuri, cha kushangaza wachezaji hao hawakuitwa na matokeo yake wameitwa wachezaji majeruhi na walioshuka kiwango hivi karibuni mfano, Kazimoto, John Bocco, Saidi juma, oscar Josha, Erasto Nyoni,.

Kwa mujibu wa mashabiki walioambatana na timu hiyo huko Afrika Kusini, wanasema kwamba sababu ya timu hiyo kufanya vibaya ni kutokuwa na ushirikiano baadhi ya viongozi walioambatana na timu hiyo na kwamwe timu haiwezi kufanya vizuri.