Friday, April 22, 2016

MCHEZAJI WA ZAMANI WA SIMBA ATOA YA MOYONI.......

Mlinzi wa zamani wa timu ya Simba SC na timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars,) Lubigisa Madata Lubigisa amesema kinachoendelea katika klabu yake hiyo ya zamani ni ‘matokeo ya ubinafsi na kutowajibika ipasavyo’ kwa uongozi wa juu ambao kwa mawazo yake (Lubigisa) wameshindwa kuwa karibu na wachezaji na kutowatimizia mahitaji yao muhimu.

Madata ambaye alikuwa sehemu ya kikosi cha timu hiyo kilichofuzu kwa hatua ya makundi ya ligi ya mabingwa Afrika mwaka 2003 amesema hayo wakati nilipomuomba mtazamo wake kuhusu mwenendo wa timu hiyo inayosotea taji la ligi kuu kwa msimu wa nne mfululizo hivi sasa.

“Kinacho endelea Simba sasahivi ni maslahi binafsi ya viongozi. Viongozi wanajali sana maslahi yao binafsi na kusahau kama jukumu lao la kuifanya Simba ishinde, kiongozi aliye makini tena wa club kubwa kama Simba anaye hitaji matokeo mazuri ili aongoze ligi hawezi kukubali kufungwa na Toto.”

“Ninachokiona kwa uongozi ni hawataki kutumia pesa ili washinde mechi kama ile, kiongozi lazima uwe karibu na wachezaji wako tumia pesa kwa wachezaji wako waahidi pesa ili wacheze kwa moyo na kujituma zaidi.”

No comments:

Post a Comment