Saturday, November 30, 2013

RATIBA:MICHEZO YA WIKI HII LIGI KUU ENGLAND

Saturday 30 November 2013

Aston VillavSunderlandVilla Park17:00
Cardiff CityvArsenalCardiff City Stadium17:00
EvertonvStoke CityGoodison Park17:00
Norwich CityvCrystal PalaceCarrow Road17:00
West Ham UnitedvFulhamBoleyn Ground17:00
Newcastle UnitedvWest Bromwich AlbionSt. James' Park19:30



Sunday 01 December 2013
Tottenham HotspurvManchester UnitedWhite Hart Lane14:00
Hull CityvLiverpoolThe KC Stadium16:05
Manchester CityvSwansea CityEtihad Stadium18:10
ChelseavSouthamptonStamford Bridge18:10
Tuesday 03 December 2013
Crystal PalacevWest Ham UnitedSelhurst Park22:00
Wednesday 04 December 2013
LiverpoolvNorwich CityAnfield21:45
Manchester UnitedvEvertonOld Trafford21:45
SouthamptonvAston VillaSt. Mary's Stadium21:45
Swansea CityvNewcastle UnitedLiberty Stadium21:45
ArsenalvHull CityEmirates Stadium21:45
Stoke CityvCardiff CityBritannia Stadium21:45
SunderlandvChelseaStadium of Light21:45
West Bromwich AlbionvManchester CityThe Hawthorns22:00
FulhamvTottenham HotspurCraven Cottage22:00









Friday, November 29, 2013

KOCHA MPYA AZAM KUSHUKA DAR MUDA WOWOTE KUJA KUANZA KAZI

KOCHA mpya wa Azam FC, Mcameroon Joseph Marius Omog aliyeipa Leopard FC ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), taji la Kombe la Shirikisho Afrika mwaka jana anatarajiwa kuwasili kesho nchini kusaini Mkataba wa kuifundisha timu hiyo.

Mchezaji huyo wa zamani wa Yaounde ni mwalimu wa kiwango cha juu cha ufundishaji soka na elimu ya viungo aliyehitimu vizuri mafunzo yake katika Chuo cha Vijana na Michezo, INJS mjini Yaounde. Alikwenda kujiendeleza kielimu nchini Ujerumani na kwa pamoja na Pierre Njili na Martin Ndtoungou walipata Stashahada za ukocha na leseni za UEFA daraja la B mwaka 1987.

 
Joseph Marius Omog, kocha mpya wa Azam FC
Aliporejea nchini mwake, Joseph Marius Omog, alifundisha timu kadhaa kama Fovu ya Baham na Aigle ya Menoua na akazifikisha fainali ya Kombe la Cameroon klabu zote. 

Mwaka 2001 aliteuliwa kuwa Msaidizi wa kocha Mjerumani, Winfried Schafer katika timu ya taifa ya Cameroon, Simba Wasiofungika chini ya Nahodha Samuel Eto’o haswa kutokana na kujua kwake Kijerumani, kwa sababu kocha huyo alikuwa hazungumzi Kiingereza wala Kifaransa. 

Mwaka 2003 aliteuliwa kuwa kocha Mkuu wa timu ya taifa baada kuondoka kwa Winfried Schafer, lakini akafukuzwa mwaka 2010 kutokana na matokeo mabaya na kushindwa kuiwezesha Cameroon kufuzu Fainali za Mataifa ya Afrika. Akaamua kutoka nje ya nchi na mwaka 2011 alijiunga na AC Leopard ya DRC na kuiwezesha kutwaa Kombe mwaka huo huo na kuipa tiketi ya kucheza Kombe la Shirikisho. 

Na akafanikiwa kuiwezesha timu hiyo kutwaa Kombe hilo la Afrika kwa kuifunga Djoliba ya Mali mabao 2-1 katika mchezo wa marudiano na kutengeneza ushindi wa jumla wa 4-3.

Kwa kifupi huyu ndiye mwalimu mpya wa Azam FC, anayekuja kurithi mikoba ya Stewart Hall, Muingereza aliyeachia ngazi mwezi uliopita.

UGANDA YAICHAPA RWANDA 1-0

BAO pekee la Dan Sserunkuma dakika ya 88, limeipa Uganda, The Cranes ushindi wa 1-0 dhidi ya Rwanda, Amavubi katika mchezo wa Kundi C Kombe la Mataifa ya Afrika Mashariki na Kati, CECAFA Challenge 2013 Uwanja wa Nyayo, Nairobi jioni hii.

Rwanda ilitawala sehemu kubwa ya mchezo na kukosa mabao mengi, lakini mwishoni mwa mchezo ikawaruhusu Uganda kuondoka na pointi tatu.
Ibrahim Salah wa Sudan akimiliki mpira mbele ya Tesmafikel Suarfael wa Eritrea leo Machakos
Wachezaji wote wa Yanga, Hamisi Kiiza alicheza upande wa Uganda na Haruna Niyonzima upande wa Rwanda.  

Katika mchezo wa kwanza, Sudan iliifunga mabao 3-0 Eritrea kwenye Uwanja wa Kenyatta, Machakos, Salah Ibrahim akifunga mawili na moja Tahir Mohammed Baada ya kukamilisha mechi za kwanza za makundi, mechi za pili zitaanza kesho Ethiopia ikimenyana na Zanzibar na Sudan Kusini na Kenya, hiyo ikiwa michezo ya Kundi A Uwanja wa Nyayo.

Katika mechi za kwanza za kundi hilo, Zanzibar iliifunga Sudan Kusini 2-1 na Kenya ilitoka sare ya bila kufungana na Ethiopia.

Thursday, November 28, 2013

RICE AGUNDULIKA KUWA NA SARATANI

Mchezaji wa zamani wa timu ya Ireland kaskazini na mlinzi wa zamani wa Arsenal Pat Rice amefikishwa hospitalini baada ya kugundulika kuwa na ugonjwa wa Saratani.

Rice mwenye umri wa miaka 64 aliichezea mara 528 timu ya washika Bunduki wa London pia aliwahi kuwa Kocha msaidizi akimsaidia Arsene Wenger kwa kipindi cha miaka 16 kabla ya kustaafu mwaka 2012.
Taarifa ya klabu ya Arsenal imethibitisha kuwa Pat yu hospitali akipata matibabu na kumtumia salamu za pole na kumtakia heri apone haraka.

Rice aliichezea Gunners kwa kipindi cha zaidi ya misimu 14 baada ya kujiunga na timu ya vijana, ambapo timu yake ilichukua ubingwa wa Kombe la Ligi na FA mara mbili ,mwaka 1971, pia alikuwa nahodha wa Timu hiyo ambayo ilipata mafanikio makubwa kwenye michuano ya FA mwaka 1979.
Wenger amesifu jitihada na kazi ya Rice ambaye alikua akifanya nae kazi mpaka alipostaafu mwaka 2012.

WAJUWE WALIOCHEZA MECHI NYINGI UEFA CHAMPIONS LEAGUE

Zlatan Ibrahimović amejiunga na listi ya wachezaji waliocheza mechi 100 au zaidi ya UEFA Champions League baada ya kuweza kuicheza timu yake ya Paris Saint-Germain katika mchezo wa kundi C game dhidi ya Olympiacos FC – na hivyo kuwa mchezaji wa 18 kufikisha idadi hiyo ya mechi. 

Mshambuliaji huyo wa kisweden amevichezea vilabu sita barani ulaya katika michuano hii, akianzia AFC Ajax, halafu Juventus, FC Internazionale Milano, FC Barcelona na AC Milan kabla ya kujiunga na PSG MSIMU ULIOPITA. Pia Zlatan ameweza kufunga jumla ya mabao 39 katika michuano hii. 

LISTI YA WACHEZAJI WALIOCHEZA MECHI NYINGI ZA UEFA CHAMPIONS LEAGUE (MAKUNDI MPAKA FINALI)142 Raúl González (Real Madrid CF, FC Schalke 04)
138 Ryan Giggs (Manchester United FC)
136 Xavi Hernández (FC Barcelona)
131 Iker Casillas (Real Madrid CF)
125 Clarence Seedorf (AFC Ajax, Real Madrid CF, AC Milan)
124 Paul Scholes (Manchester United FC)
120 Roberto Carlos (Real Madrid CF, Fenerbahçe SK)
115 Carles Puyol (FC Barcelona)
112 Thierry Henry (AS Monaco FC, Arsenal FC, FC Barcelona)
109 Paolo Maldini (AC Milan)
109 Gary Neville (Manchester United FC)
107 David Beckham (Manchester United FC, Real Madrid CF, AC Milan, Paris Saint-Germain)
104 Víctor Valdés (FC Barcelona)
103 Oliver Kahn (FC Bayern München)
103 Luís Figo (FC Barcelona, Real Madrid CF, FC Internazionale Milano)
102 Ashley Cole (Arsenal FC, Chelsea FC)
100 Andriy Shevchenko (FC Dynamo Kyiv, AC Milan, Chelsea FC)
100 Zlatan Ibrahimović (AFC Ajax, Juventus, FC Internazionale Milano, FC Barcelona, AC Milan, Paris Saint-Germain)
99 Alessandro Nesta (SS Lazio, AC Milan)
99 Petr Čech (AC Sparta Praha, Chelsea FC)
98 Andrea Pirlo (FC Internazionale Milano, AC Milan, Juventus)
98 Edwin van der Sar (AFC Ajax, Juventus, Manchester United FC)
97 Guti (Real Madrid CF)
97 Javier Zanetti (FC Internazionale Milano)
96 Claude Makelele (FC Nantes, Real Madrid CF, Chelsea FC)
96 Cristiano Ronaldo (Manchester United FC, Real Madrid CF)
96 Frank Lampard (Chelsea FC)

TENGA AENDA KIKAO FIFA, LAKINI HAKURIDHISHWA NA HALI ALIYOIACHA KOMBE LA CECAFA

KILI STARS YATOKA SARE NA ZAMBIA HUKU BURUNDI IKISHINDA 2-0 DHIDIYA SOMALIA

TANZANIA Bara, Kilimanjaro Stars imeanza taratibu michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika Mashariki na Kati, CECAFA Challenge baada ya kutoa sare ya 1-1 na mabingwa wa zamani wa Afrika, Zambia au Chipolopolo kwenye Uwanja wa Kenyatta, Machakos, Kenya.
Katika mchezo huo wa Kundi B, Zambia ndiyo waliokuwa wa kwanza kupata bao kupitia kwa Ronald Kampamba dakika ya 41, akiunganisha kwa kichwa krosi ya Felix Katongo.
Zambia walitawala zaidi mchezo huo kipindi cha kwanza na kutengeneza nafasi zaidi ya nne za kufunga, lakini sifa zimuendee kipa Ivon Philip Mapunda aliyeokoa michomo kadhaa ya hatari.


Kipindi cha pili, Stars ilibadilika mno kiuchezaji, japokuwa wachezaji waliomaliza kipindi cha kwanza ndiyo wote waliorejea kuanza ngwe hiyo ya lala salama.
Kutokana na mshambulizi mfululizo langoni mwa Zambia, Bara walipata kona dakika ya 48 ambayo ilikwenda kuchongwa na Salum Abubakar ‘Sure Boy’ na kuunganishwa nyavuni na Said Morad kwa kichwa.
Baada ya bao hilo, Zambia walianza kuutafuta mpira kwa tochi na kama si umahiri wa kipa wao, Nsabata Toaster kuokoa hatari nyingi, Stars wangeweza kuondoka na ushindi.  
Kwa matokeo hayo, Burundi inaongoza kundi hilo baada ya kuifunga Somalia 2-0 katika mchezo wa kwanza wa kundi hilo kwenye Uwanja huo. 
Kikosi cha Stars kilikuwa; Ivo Mapunda, Himid Mao, Erasto Nyoni, Said Morad, Kevin Yondan, Frank Domayo, Salum Abubakar ‘Sure Boy’/Ramadhani Singano ‘Messi’ dk89, Hassan Dilunga/Athumani Iddi ‘Chuji’ dk85, Elias Maguri/Haroun Chanongo dk72, Amri Kiemba na Mrisho Ngassa.
Chipolopolo; Nsabata Toaster, Bronson Chama, Jimmy Chisenga/Kabaso Chongo dk67, Christopher Munthali, Rodrcik Kabwe, Stanley Nshimbi/Alex Nshimbi dk57, Sydney Kalume, Kondwani Mtonga, Felix Katongo/Salulani Phiri dk73, Ronald Kampamba na Festus Ndewe.

Wednesday, November 27, 2013

MANCHESTER UNITED WAJIANDAA KUMSAJILI BENDER

Manchester united huwenda ikajiuliza baada ya kufeli katika harakati za usajili wa kiungo bora ili kuja kuisaidia safu ya kiungo ya timu hiyo ambayo imekuwa ikiyumba katika kipindi kirefu sasa hasa baada ya kustaafu kwa Paul Scholes.

Katika kulifanikisha hilo man united wapo katika harakati kupitia kwa kocha wa timu hiyo ili kumsajili kiungo kutoka ujerumani na timu ya Bayern Leverkusen Las Bender ambaye leo usiku atakuwa miongoni mwa kizingiti kikubwa katika safu ya kiungo.

Moyes yupo katika kumuangalia kiungo huyo mwenye miaka 24 leo ili kuongeza nia yake ya kumsajili kiungo huyo ambaye amekuwa gumzo ndani ya timu ya Arsenal.

KOLO TOURE AMFAGILIA MDOGO WAKE YAYA TOURE, ASEMA YAYA NI BORA KULIKO BUSQUETS

Beki wa kati wa liverpool na tiu ya taifa ya Iviry Coast amesema kwamba Barcelona ilifanya uwamuzi usiostahili kumuuza mdogo wake Yaya Toure.

Beki huyo anaamini kwamba Yaya ni bora kuliko Busquets na wamefanya kosa ambalo hawatokuja kulifanya tena.

Mkongwe huyo ameendelea kusema kwamba Yaya ni kiungo bora kwa sasa duniani na huwezi kumlinganisha na Busquets kwa sasa na hilo linathibitika sasa kwani Yaya ndio tegemezi katika kikosi cha Man city kwa sasa..

Kolo toure kwa sasa yupo na timu ya liverpool na aafanya vizuri katika kikosi hicho kinachosshika nafasi ya pili katika msimamo wa ligi kuu ya England.

KILIMANJARO STARS YAENDELEA NA MAZOEZI KATIKA HALI NZURI HUKU KIM POLSEN AKITARAJIA KUWAANZISHA NGASSA NA MAGURI

KOCHA Mdenmark Kim Poulsen wa timu ya Bara, Kilimanjaro Stars anatarajiwa kuwaanzisha pamoja katika safu ya ushambuliaji Mrisho Ngassa wa Yanga SC na Elias Maguri wa Ruvu Shooting katika mchezo wa ufunguzi wa Kundi B, Kombe la Mataifa ya Afrika Mashariki na Kati, CECAFA Challenge dhidi ya Zambia kesho Machakos, Kenya.

Katika mazoezi ya leo asubuhi ya Stars inayodhaminiwa na bia ya Kilimanjaro Premium Lager, Uwanja wa Chuo Kikuu cha Strathmore, Nairobi imeonyesha Kim atawaanzisha Himid Mao, Erasto Nyoni, Said Morad wote wa Azam FC kwa pamoja na Kevin Yondan wa Yanga katika safu ya ulinzi.

Kim ataanzisha viungo watatu mafundi watupu, Hassan Dilunga wa Ruvu Shooting aliyesaini Yanga kwa ajili ya dirisha dogo, Frank Domayo wa Yanga na Salum Abubakar ‘Sure Boy’ wa Azam FC wakati washambuliaji watakuwa Ngassa na Maguri.

Akizungumza baada ya mazoezi, kocha huyo alisema kwamba maandalizi yake ni mazuri na anatarajia upinzani mkali katika mchezo wa kesho kwa kuwa Zambia ni timu nzuri.

“Kila kitu ni safi, tumejiandaa vizuri tangu Dar es Salaam, hapa leo tulikuwa tunaamsha misuli tu, na tumejiandaa kwenda kucheza mchezo wa kushambulia moja kwa moja, vijana wanaonyesha wako tayari na jambo la kufurahisha kwangu, tutacheza kwenye Uwanja wa nyasi bandia, kama wa Karume (Dar es Salaam) tuliokuwa tunafanyia mazoezi,”alisema.

Kim alisema kwamba anataka kutumia mashindano haya kutambulisha wachezaji wapya ili kukuza uwigo wa wachezaji wa timu ya muungano, Taifa Stars ambayo pia yeye ndiye kocha wake Mkuu.

“Nafurahi nitawaona Zanzibar hapa, nitaona wachezaji wao kwa ajili ya kutafuta wachezaji wa Taifa Stars na pia nipo na Kilimanjaro Stars, hii ni fursa nzuri kwangu,”alisema.
 
Kim amesistiza mashindano haya ya Challenge timu nyingi zinayatumia kutambulisha wachezaji wapya, hivyo naye ameamua kufanya hivyo pia.        
Kuhusu mazingira kwa ujumla kuanzia hoteli waliyofikia Sandton na Uwanja wa mazoezi, Kim amesema ameridhishwa navyo na hawezi kutarajia makubwa zaidi ya hayo kulingana na halisi ya CECAFA. 
 
Anafurahi zaidi timu yake haina majeruhi hata mmoja na baada ya mazoezi ya takriban saa mbili leo Strathmore, Kim aliondoka na wachezaji wake kwenda kupumzika hotelini, kuweka fikra zao sawa kuelekea mchezo wa kesho.
 
Stars kesho itawakosa washambuliaji Mbwana Samatta na Thomas Ulimwengu, ambao wanasubiri kuichezea klabu yao, TP Mazembe ya DRC Fainali ya pili ya Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya Sfaxien ya Tunisia Novemba 30 mjini Lubumbashi na Desemba 1, watakuja Nairobi kuungana na wenzao. 
 
Huu ni mwaka wa pili mfululizo Kim anaiongoza Kilimanjaro Stars katika mashindano haya, baada ya mwaka jana nchini Uganda, ambako waliambulia nafasi ya nne baada ya kufungwa kwa penalti na Zanzibar. 
 
Stars inaingia kwenye Challenge ya mwaka huu, ikiwa na kumbukumbu ya kutwaa mataji matatu ya mashindano hayo katika miaka ya 1974 mjini Dar es Salaam, 1994 mjini hapa na 2010 Dar es Salaam pia.
 
Michuano ya Challenge inaanza rasmi mchana wa leo, Zanzibar wakifungua dimba kwa kumenyana na Sudan Kusini Uwanja wa Nyayo kabla ya wenyeji Kenya kumenyana na Ethiopia jioni.


MAN UNITED WANUSURIKA NA AJALI YA NDEGE WAKIELEKEA UJERUMANI LEO

KOCHA David Moyes na kikosi chake cha Manchester United walipatwa na mshituko wakiwa angani Ujerumani jana kwa safari ya mchezo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Bayer Leverkusen baada ya ndege hiyo kughairi kutua Uwanja wa Ndege wa Cologne.
 
Ndege ya United ilikuwa umbali wa mita 400 kuelekea chini Uwanja wa Ndege wa Cologne wakati Rubani alipofoka akisema kuna ndege nyingine katika eneo alilotaka kutua.
 
Wakati wachezaji wa klabu hiyo ya Ligi Kuu ya England wakirejea kwenye siti zao, Rubani akalazimika kuzunguka upande mwingine kuishusha ndege hiyo
Wametulia: Ashley Young na Jonny Evans wakiwa Uwanja wa ndege wa Manchester kabla ya safari ya Ujerumani
Hairy moment: Rio Ferdinand tweeted that he had 'just recovered from a choppy landing'
Rio Ferdinand ametweet juu ya kutua kwao salama
David Moyes
Wayne Rooney
David Moyes na Wayne Rooney Uwanja wa Ndege wa Manchester

Kikosi kizima cha United, wakiwemo wachezaji, kocha David Moyes na viongozi wote wa benchi la Ufundi walikuwa kwenye ndege na beki Rio Ferdinand akatweet baada ya kutua: "Tumetua Ujerumani...baada ya kupatwa msukosuko hivi wakati wa kutua.’
Sir Bobby Charlton, ambaye alikuwepo katika msafara wa United uliopata ajali mjini Munich mwaka 1958, na Sir Alex Ferguson hawakuwamo kwenye ndege hiyo
All smiles: David Moyes was happy enough when he gave a press conference in Germany
David Moyes alikuwa mwenye furaha kiasi cha kutosha baada ya kutua Ujerumani wakati anazungumza na Wandishi wa Habari
Cheery: Chris Smalling was also in buoyant mood despite the air scare
Chris Smalling alikuwa kwenye hali nzuri pia

ZANZIBAR YAANZA VIZURI MICHUANO YA CHALLENGE, YAICHAPA SUDAN KUSINI 2-1

ZANZIBAR imeanza vyema michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika Mashariki na Kati, CECAFA Challenge baada ya kuifuga mabao 2-1 Sudan Kusini katika mchezo wa ufunguzi wa Kundi A, Uwanja wa Nyayo, Nairobi, Kenya.

Mabao ya Zanzibar Heroes leo yalfungwa na kiungo wa Coastal Union ya Tanga, Suleiman Kassim ‘Selembe’ dakika ya saba baada ya kuipangua ngome ya Sudan Kusini na kufumua shuti lililomshinda kipa Juma Jinaro na Adeyoum Saleh Ahmed dakika ya 67.

Bao la Sudan Kusini lilifungwa na Fabiano Lako dakika ya 73, zikiwa ni dakika tano aiingie kuchukua nafasi ya Francis Khamis.

Zanzibar ingeweza kuondoka na ushindi mnene leo kama washambuliaji wake, Khamis Mcha ‘Vialli’ na Ally Badru wangetumia vyema nafasi nzuri walizopata. Nafasi nzuri zaidi ambayo Zanzibar walipata ilikuwa dakika ya 43 baada ya Badru kumlamba chenga kipa, lakini Khamis Mcha alipopiga pira ukagonga mwamba na kipa akaudaka.

Zanzibar; Abdallah Rashid, Salum Khamis/Ally Khan dk78, Waziri Salum, Shaffi Hassan, Mohamed Fakhi, Sabri Ali, Masoud Ali, Suleiman Kassim, Awadh Juma na Khamis Mcha/Amour Omar dk44/Adeyoum Saleh dk62. 

Sudan Kusini; Juma Jinaro, Atar Thomas, Philip Delfino, Edomon Amadeo, Richard Justin, Wiiam Offiri, Jimmy Erasto, Thomas Jacob, Godfrey Peter, Francis Khamis/Fabiano Lako dk68 na James Joseph.

Tuesday, November 26, 2013

KILI STARS YAWASILI SALAMA KENYA, TAYARI KWA MICHUANO YA CECAFA CHALLENGE CUP

Timu ya Tanzania Bara (Kilimanjaro Stars) imewasili salama Nairobi, Kenya tayari kwa mashindano ya Kombe la Chalenji yanayoanza kesho (Novemba 27 mwaka huu) katika Uwanja wa Nyayo.

Kilimanjaro Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager iliwasili saa 3 usiku kwa ndege ya RwandAir, na imefikia katika hoteli ya Sandton iliyoko katikati ya Jiji la Nairobi.

Kwa mujibu wa programu ya Kocha Mkuu Kim Poulsen, Kilimanjaro Stars leo (Novemba 26 mwaka huu) ni mapumziko ambapo kesho itafanya mazoezi kujiandaa kwa mechi yake ya kwanza dhidi ya Zambia itakayochezwa Novemba 28 mwaka huu Uwanja wa Machakos.

TANZANITE VS AFRIKA KUSINI HATIMAYE KUCHEZWA DAR

MECHI ya kwanza ya Raundi ya michuano ya Kombe la Dunia, Kanda ya Afrika kwa wanawake chini ya miaka 20 kati ya Tanzania (Tanzanite) na Afrika Kusini iliyokuwa ichezwe Mwanza sasa itafanyika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Baada ya ukaguzi uliofanywa na maofisa wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), imebainika uwanja huo unatakiwa ufanyiwe marekebisho ambayo hayawezi kuwahi Desemba 7 mwaka huu, siku ambayo ndiyo mechi hiyo inatakiwa kuchezwa.

Vyumba vya wachezaji vya Uwanja huo ndilo eneo ambalo linatakiwa  kufanyiwa marekebisho makubwa.

CECAFA YAPATA VIONGOZI WAPYA , MALINZI AWA MJUMBE

BARAZA la Vyama vya Soka Afrika Mashariki na Kati (CECAFA), limepata Wajumbe wapya wanne wa Kamati ya Utendaji katika uchaguzi mdogo uliofanyika jana hoteli ya Hillpack, Nairobi, Kenya.

Akizungumza na Waandishi wa Habari mchana wa leo katika hoteli ya Hillpack, Rais wa CECAFA, Mtanzania Leodegar Chillah Tenga amesema kwamba uchaguzi huo umefanyika kidemokrasia na washindi wamepatikana kihalali.

Wajumbe waliochaguliwa ni Lawrence Mulindwa kutoka Uganda, aliyepata kura 12, Tariq Atta wa Sudan kura 10, Abdigan Said wa Somalia kura tisa na Raoul Gsanura wa Rwanda aliyepata kura nane.
 
Walioangushwa ni Chabur Alex wa Sudan Kusini aliyepata kura tano na Sam Nyamweya wa Kenya aliyepata kura nne.
 
Pamoja na hayo, Tenga ameipongeza Kenya kwa kuwa mwenyeji wa Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika Mashariki na Kati, CECAFA Challenge mwaka huu.

Rais Tenga amesema kwamba pamoja na jitihada za CECAFA kuandaa michuano ya wakubwa ya Challenge, wanatakiwa pia kufanya mashindano ya vijana na wanawake, ili kukuza soka ya ukanda huu.
        
Michuano ya CECAFA Challenge inaanza  na Zanzibar itafungua dimba na Sudan Kusini saa 8:00 mchana kabla ya wenyeji, Kenya kucheza na Ethiopia saa mbili baadaye, Uwanja wa Nyayo.
 
Tanzania Bara, Kilimanjaro Stars itacheza na Zambia saa 10:00 jioni ya keshokutwa baada ya mechi kati ya Burundi na Somalia itakayoanza saa 8:00 mchana Uwanja wa Machakosi.  

WAKATI DIRISHA DOO LA USAJILI BARA LIKITARAJIWA KUFUNGWA DECEMBER 15, SIMBA YA MSAINISHA RASMI KIUNGO KUTOKA MTIBWA

USAJILI wa dirisha dogo la usajili linafungwa Desemba 15 mwaka huu, Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) tunazikumbusha klabu zote kuheshimu kanuni na kuzingatia muda uliowekwa.

Pia tunakumbusha kuwa kupeleka mchezaji kwa mkopo katika klabu nyingine hakutoi nafasi ya kusajili mchezaji mpya. Kama klabu ilisaji wachezaji 30 maana yake ni kuwa haina nafasi ya kuongeza wachezaji.

 Kwa upande wa wachezaji wa kigeni (foreign players), tunakumbusha kuwa kuanzia msimu ujao 2014/2015 watakuwa watatu tu badala ya watano wa sasa. Kuhusu usajili wa wachezaji kutoka nje mpaka sasa hakuna hata klabu moja imeshaingia kwenye TMS kuomba uhamisho. Itakapofika Desemba 15, system ya TMS itafunga. Wakati huo huo: TFF imepokea kwa masikitiko taarifa za kifo cha mwamuzi wa zamani wa FIFA, Andrew Kiloyi kilichotokea mjini Iringa. Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa Chama cha Waamuzi wa Mpira wa Miguu Mkoa wa Iringa, Ramadhan Mahano, Kiloyi alifariki dunia juzi (Novemba 24 mwaka huu) kutoka na ugonjwa wa fangasi ya ubongo, na marehemu amesafirishwa kwenda kwao Kigoma ambapo atazikwa.

Kiloyi alizaliwa Mei 5, 1968. Alijiunga na uamuzi wa mpira wa miguu mwaka 1988 ambapo alipata beji ya FIFA mwaka 2001 akiwa mwamuzi msaidizi. Alistaafu uamuzi mwaka 2009, na hadi anafariki akiwa mjumbe wa Kamati ya Waamuzi ya Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Iringa (IREFA).

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) linatoa pole kwa familia ya marehemu, IREFA, ndugu, jamaa na marafiki kutokana na msiba huo na kuwataka kuwa na moyo wa subira na uvumilivu katika kipindi hicho cha majonzi. Mungu aiweka mahali pema roho ya marehemu Kiloyi.

Monday, November 25, 2013

BAADA YA KUONGEZA MKATABA WA KUICHEZEA YANGA BEKI YONDANI ACHAGULIWA KUWA NAHODHA WA STARS HUKU IKIAGWA LEO MCHANA

KOCHA Mkuu wa timu ya taifa ya Bara, Kilimanjaro Stars, Kim Pouslen amemtambulisha beki Kevin Yondan kuwa Nahodha mpya wa timu hiyo, anayechukua nafasi ya Juma Kaseja aliyeachwa kwenye kikosi hicho kinachoondoka jioni ya leo kwenda Nairobi, Kenya kushiriki michuano ya Kombe la Challenge inayoanza kutimua vumbi Novemba 27 mwaka huu.

 Stars imeagwa leo mchana kwa hafla fupi kambini kwao katika hoteli ya Accomondia jijini Dar es Salaam na kukabidhiwa bendera na Katibu wa Baraza la Michezo la Taifa (BMT), Henry Lihaya. 

Kocha wa Stars, Mdenmark Poulsen amesema kwamba anakwenda Kenya kwa lengo moja kubwa kupigana kukata tiketi ya kucheza Robo Fainali kutoka kwenye Kundi lao B, na baada ya hapo mapambano mengine yatafuatia. Amesema anafurahi wachezaji wake wako tayari sana kwa ajili ya mashindano hayo na wamemuahidi kufanya vizuri.\

Nahodha mpya, Yondan kwa upande wake amesema kwamba amefurahia wadhifa huo na kwa pamoja na wachezaji wenzake, wanaahidi kwenda kupigana kurejesha heshima ya timu yao iliyopotea kwa sasa.

“Tunaahidi kwenda kupigana na Mungu atatujaalia tutarudi na Kombe na kurudisha heshima yetu, kwa sababu timu yetu kwa sasa  ni kama imeshuka hivi na kupoteza heshima yake mbele ya wananchi, ila tukirudi na Kombe hapa, heshima itarudi,”alisema.
Mkuu wa Msafara, Geoffrey Nyange ‘Kaburu’ amesema wanakwenda Nairobi, Kenya kupigana kwa nguvu zote kuhakikisha Kombe la Challenge linakuja Dar es Salaam.
 
Msafara wa Stars iliyotwaa Kombe la Challenge mara tatu, 1974, 1994 na 2010, utaondoka saa 10:00 jioni kwa ndege ya RwandAir.
 
Wachezaji waliomo katika msafara huo ni makipa Deogratius Munishi (Yanga), Ivo Mapunda (Gor Mahia, Kenya) na Aishi Manula (Azam). Mabeki ni Erasto Nyoni (Azam), Himid Mao (Azam), Ismail Gambo (Azam), Kelvin Yondani (Yanga), Michael Pius (Ruvu Shooting) na Said Moradi (Azam).
 
Viungo ni Amri Kiemba (Simba), Athuman Idd (Yanga), Frank Domayo (Yanga), Haruna Chanongo (Simba), Hassan Dilunga (Ruvu Shooting), Ramadhan Singano (Simba) na Salum Abubakar (Azam).
 
Safu ya ushambuliaji inaundwa na Elias Maguli (Ruvu Shooting), Faridi Musa (Azam), Joseph Kimwaga (Azam), Juma Liuzio (Mtibwa Sugar), Mbwana Samata (TP Mazembe, DRC), Mrisho Ngasa (Yanga) na Thomas Ulimwengu (TP Mazembe, DRC).

ZIJUE JEZI MPYA ZA BRAZIL ZITAKAZOTUMIKA KWENYE FAINALI ZA KOMBE LA DUNIA






YANGA WAMPIGA PINGU YONDANI, ASAINI MKATABA MPYA

KLABU ya Yanga SC imemuongezea Mkataba wa miaka miwili beki wake Kevin Patrick Yondan, ambaye alikuwa ananyemelewa na klabu yake ya zamani, Simba SC.

Yondan alisaini Mkataba huo juzi mjini Dar es Salaam na sasa atakuwa mali ya Yanga hadi Juni 2016.

Juni mwakani, Yondan alikuwa anamaliza Mkataba wake wa awali Yanga SC wa miaka miwili na kwa ndoa mpya- maana yake kuna uwezekano mchezaji huyo bora Mambo yanamuendea vizuri Yondan tangu ajiunge na Yanga SC, kwani mbali na kushinda tuzo ya Mchezaji Bora wa Ligi Kuu msimu uliopita, pia leo ameteuliwa kuwa Nahodha wa kikosi cha Bara, Kilimanjaro Stars. 
 
Kocha wa Stars, Kim Pouslen amemtambulisha Yondan kuwa Nah
odha mpya wa timu hiyo, anayechukua nafasi ya Juma Kaseja aliyeachwa kwenye kikosi hicho kinachoondoka jioni ya leo kwenda Nairobi, Kenya kushiriki michuano ya Kombe la Challenge inayoanza kutimua vumbi Novemba 27 mwaka huu.
Stars imeagwa leo mchana kwa hafla fupi kambini kwao katika hoteli ya Accomondia jijini Dar es Salaam na kukabidhiwa bendera na Katibu wa Baraza la Michezo la Taifa (BMT), Henry Lihaya.wa Ligi Kuu msimu uliopita atamalizia soka yake Jangwani.

VIDE: MANCITY IKIINYUKA SPURS 6-0

VIDEO: MAN UNITED IKITOKA DRAW JANA DHIDI YA CARDIFF CITY

Sunday, November 24, 2013

TP MAZEMBE YAPOTEZA FAINALI YA KWANZA YACHAPWA 2-0 TUNISIA

TIMU ya soka ya CS Sfaxien ya Tunisia, Jana imeutumia vyema Uwanja wa nyumbani, Stade Olympique de Rades baada ya kuilaza mabao 2-0  Tout Puissant Mazembe ya DRC katika Fainali ya kwanza ya Kombe la Shirikisho Afrika mjini Tunis.

Shukrani kwao, washambuliaji wa kimataifa wa Gabon, Ibrahim Didier Ndong aliyefunga bao la kwanza dakika ya 16 na mshambuliaji wa Taha Yassine Khenissi aliyefunga la pili dakika ya 90 na ushei wakimtungua kipa mahiri, Robert Muteba Kidiaba.

 Washambuliaji wote wa Tanzania, Mbwana Ally Samatta na Thomas Emanuel Ulimwengu walianza katika kikosi cha Mazembe pamoja na Tressor Mputu Mabi, lakini hawakuweza kuwanusuru mabingwa mara nne Afrika na kipigo hicho.Sfaxien, timu pekee iliyoshinda Kombe la Shirikisho mara mbili tangu kutambulishwa kwa mfumo mpya mwaka 2004, yenye maskani yake katika mji uliozungukwa na bahari ya Mediterranean, Sfax sasa itahitaji sare katika mchezo wa marudiano Novemba 30 au kufungwa kwa tofauti isiyozidi bao 1-0, mjini Lubumbashi ili kujinyakulia taji na kitita cha dola za Kimarekani, 625 000. Mshindi wa pili atapata dola 432 000. 

Mshindi pia atamenyana na mabingwa wa Ligi ya Mabingwa, Al Ahly ya Misri kuwania taji la Super Cup mechi itakayopigwa nchini Misri Februari 2014.

CRISTIANO RONALDO APATA MAJERAHA JANA , MADRID IKISHINDA 5-0

REAL Madrid imeibuka na ushindi wa mabao 5-0 usiku huu dhidi ya Almeria katika Ligi Kuu ya Hispania, maarufu kama La Liga kwenye Uwanja wa Estadio de los Juegos, Mediterráneos.
Cristiano Ronaldo alifunga bao la kwanza dakika ya tatu kwa Real Madrid pasi ya Isco kabla ya kutolewa nje kwa maumivu ya nyama, ambayo kwa sasa yanamuweka nje mpinzani wake mkuu katika tuzo ya Mwanasoka Bora wa Dunia, Lionel Messi wa Barcelona pia ya Hispania.
Sasa Mreno huyo yuko shakani kuichezea Real katika mechi ya Ligi ya Mabingwa dhidi ya Galatasaray Jumatano, ingawa baada ya mechi kocha wa Madrid , Carlo Ancelotti alisema: "Cristiano ana matatizo ya nyama, lakini ni mshituko tu, hakuna maumivu makubwa,". 
Karim Benzema aliifungia Real bao la pili dakika ya 61 pasi ya Jese Rodriguez kabla ya Gareth Bale kufunga la tatu dakika ya 71, , Isco la nne dakika ya 75 pasi ya Jese Rodriguez na Alvaro Morata kuhitimisha karamu hiyo ya mabao dakika ya 81, pasi ya Casemiro.
Still going: Real are trying to keep pace with Barcelona at the top of La Liga

 
Pace and power: Real Madrid's Cristiano Ronaldo skips past Almeria's Jesus Joaquin Fernandez

In the goals: Xabi Alonso congratulates Ronaldo after the Portugal man scored

Wizard: Bale takes a tumble as Real go on search for another goalTricky player: Real midfielder Isco gets past Almeria's Verza

Another: Karim Benzema scored Real's second in there easy win

PACQUIAO MOTO JUU , AMTANDIKA MTU MWANZO MWISHO MAYWEATHER ASUBIRIWA

BONDA Manny Pacquiao amerejesha heshima baada ya kumpiga kwa pointi Brandon Rios mjini Macau asubuhi ya leo.
Mfilipino huyo alirejea ulingoni baada ya mwaka mmoja tangu apigwe kwa Knockout na Juan Manuel Marquez.
Na alishinda kila raundi hivyo kuweka hai matumaini ya kupigana katika pambano la dola za Kimarekani 300 dhidi ya Floyd Mayweather Jnr.
Alipata pointi 10 dhidi ya tisa kila Raundi katika Raundi 10 na mwisho wa siku akakusanya pointi 120 kwa 109.
Amerudi! Manny Pacquiao ameshinda kiulaini kwa pointi dhidi ya Brandon Rios mjini Macau Jumapili ya leoComfortable: Pacquiao (right) was never in danger against the rugged but limited Rios
Comfortable: Pacquiao (right) was never in danger against the rugged but limited Rios
Can't miss: Pacquiao's speed and movement bewildered Rios as the American failed to stamp his authority
 
 
Can't miss: Pacquiao's speed and movement bewildered Rios as the American failed to stamp his authority
Bouncing back: Pacquiao responded well to back-to-back defeats to Juan Manuel Marquez and Timothy Bradley
Bouncing back: Pacquiao responded well to back-to-back defeats to Juan Manuel Marquez and Timothy Bradley