Sunday, January 26, 2014

ZAHA , FABIO KWENDA CARDIFF CITY KWA MKOPO

WACHEZAJI wawili wa Manchester United, Wilfried Zaha na Fabio Da Silva wapo karibu kujiunga na Cardiff City.
Winga wa United, Zaha amekwenda kufanyiwa vipimo vya afya St George Park kuekelea kukamilisha uhamisho wa mkopo hadi mwishoni mwa msimu, wakati bek Fabio anatarajiwa kusaini Mkataba wa moja kwa moja.
Zaha amekuwa akitakiwa na Cardiff tangu Oktoba na sasa ndoto za klabu hiyo kumpata nyota huyo zinatimia.    



Sunday, January 12, 2014

YAYA TOURE NDIYO BABA LAO AFRIKA

Mchezaji wa Manchester City ambaye pia hucheza nafasi ya kiungo cha kati katika timu ya Ivory Coast, Yaya Toure ndiye mwanasoka bora zaidi mwaka 2013 barani Afrika
Toure alikabidhiwa tuzo la (caf) mwaka wa tatu mfululizo katika sherehe zilizofanyika mjini Lagos, Nigeria Alhamisi usik

Aidha Toure pia alishinda tuzo la BBC la mwanasoka bora zaidi barani Afrika mwaka jana.
Alikuwa anawania tuzo hilo dhidi ya mchezaji mwenzake wa Ivory Coast Didier Drogba, ambaye huchezea Galatasaray na John Mikel Obi mnigeria ambaye husakata soka nchini Uingereza.

"nimefurahi sana kwa sababu hii ni ishara kuwa nacheza vyema sana ,'' alisema Toure baada ya kupokea tuzo yake.
Lakini alisema kuwa majaji walikuwa na wakati mgumu kumchagua mchezaji bora kwa sababu washindani wenzake wote ni wazuri.

''Sikudhani kama nitashinda kwa sababu Drogba na Obi Mikel ni wasakataji wazuri wa kabumbu,'' aliongeza Toure.
Washidi wa hivi karibuni wa tuzo ya Caf
2013 Yaya Toure
2012 Yaya Toure
2011 Yaya Toure
2010 Samuel Eto'o
2009 Didier Drogba
2008 Emmanuel Adebayor
2007 Frederic Kanoute
2006 Didier Drogba 


Abedi Pele wa Ghana alishinda tuzo hiyo mara tatu kati ya mwaka 1991-93 huku Samuel Eto'o akishinda kati ya mwaka 2003-05.

Bila shaka klabu ya Man City anakosakatia kambumbu Toure, bado haishinda kombe lolote la klabu lakini nyota yake imekuwa iking'aa sana nyumbani na katika nyanja za kimataifa.

Toure ndiye mchezaji pekee wa kiafrika kuwa katika orodha ya wachezaji 23 walioteuliwa kuwania tuzo la mchezaji bora la FIFA mwaka jana.

Mshindani wake wa karibu aliyekuwa pia anawania tuzo la Caf, Mikel, mwenye umri wa miaka 26, alisaidia Nigeria kushinda kombe la taifa bingwa Afrika mwaka 2013 nchini Afrika Kusini.

HATIMAYE MAN UNITED YAZINDUKA YAICHAPA SWANSEA 2-0

KOCHA David Moyes amepumua kidogo baada ya Manchester United kushinda 2-0 dhidi ya Swansea City usiku huu Uwanja wa Old Trafford na kuepuka kipigo cha nne mfululizo na cha tatu Uwanja wa nyumbani. 
Ushindi wa United leo katika mchezo huo wa Ligi Kuu ya England umetokana na mabao ya Antonio Valencia dakika ya 47 na Dany Welebeck dakika ya 59
United sasa inatimiza pointi 37 baada ya kucheza mechi 21, ingawa inabaki nafasi ya saba kwenye msimamo.

Ahead: Valencia celebrates after putting United 1-0 up just after the break at Old Trafford

JAMALI MALINZI NA MWANZO WAKE WA KUKEMEA DAWA ZA KULEVYA

RAIS wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Jamal Malinzi amezindua programu ya kutoa elimu ya kupambana na matumizi ya dawa za kulevya kwa vijana iitwayo Ishi Huru.

Programu hiyo iliyozimduliwa jana (Januari 10 mwaka huu) jijini Dar es Salaam iko chini ya taasisi ya Africa Inside Out inayoongozwa na Rebecca Young wakati washirika (partners) ni TFF na kampuni ya Rhino Resources ya Marekani.



Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Jamal Malinzi akizungumza kwenye uzinduzi wa programu ya Ishi Huru jijini Dar esSalaam.

Rais Malinzi amesema matumizi ya dawa za kulevya nchini yamekuwa yakiongezeka, hivyo kuwa kikwazo kwa maendeleo ya vijana ambapo ameipongeza Africa Inside Out kwa programu hiyo kwa vile itazuia vijana
wengi kujiingiza katika matumizi ya dawa hizo.

“Moja athari kubwa za matumizi ya dawa za kulevya ni kupata maambukizi ya virusi vya Ukimwi kutokana na kuchangia sindano za kujidunga dawa hizo.

“TFF tutatoa ushirikiano wa kutosha katika programu hii. Lakini pia tutaingiza Ishi Huru katika programu zetu za mpira wa miguu kwa vijana. Tutahamasisha jamii katika kupambana na dawa za kulevya,” amesema.

Katika uzinduzi huo, pia Rais Malinzi alizundua semina ya waelimishaji na kuwaeleza kuwa wamepata fursa hiyo kwa vile ni vijana wanaojituma, hivyo watafikisha vizuri ujumbe wa Ishi Huru katika shule na vituo vya vijana.

Friday, January 10, 2014

SIMBA NOMA SAAAAANA..!!! YAICHAPA URA 2-0 BILA HURUMA NA KUTINGA FAINALI KOMBE LA MAPINDUZI

SIMBA SC wamefuzu kuingia Fainali ya Kombe la Mapinduzi, baada ya usiku huu kuilaza mabao 2-0 URA ya Uganda kwenye Uwanja wa Amaan, Zanzibar. Shujaa wa Simba SC leo alikuwa ni kiungo mwenye kipaji, Amri Ramadhani Kiemba aliyesababisha bao la kwanza na kufunga mwenyewe la pili. URA ilipata pigo mapema dakika ya 32 baada ya mshambuliaji wake hatari, Owen Kasuule kutolewa nje kwa nyekundu ya moja kwa moja kwa kumchezea rafu winga msumbufu wa Simba SC, Ramadhani Singano ‘Messi’.
Kiemba akipongezwa na wenzake baada ya kufunga bao la pili
Dakika 45 za kipindi cha kwanza zilimalizika timu hizo zikiwa hazijafungana na kipindi cha pili ndipo Simba SC inayofundishwa na Mcroatia, Zdravko Logarusic ilipofungua makucha yake.    Kona maridadi ya Kiemba ilimkuta beki Donald Mosoti, aliyemsetia beki pacha wake wa kati, Joseph Owino akafunga bao la kwanza dakika ya 49. Wakati URA wanahaha kusaka bao la kusawazisha, Simba SC walifanya shambulizi zuri na krosi maridadi ya Haroun Chanongo ikaunganishwa nyavuni na Amri Kiemba dakika ya 52 kuipatia Simba SC bao la pili. Bao hilo liliinyong’onyesha kabisa URA, ingawa iliendelea kupambana kupata japo bao la kufutia machozi. Kwa ujumla, URA iliathiriwa mno na kutolewa na mshambuliaji wake hatari, Owen Kasuule, kwani ndiye tegemeo lake la mabao kwa pamoja na Feni Ali. Baada ya mechi, Kiemba alipewa king’amuzi cha Azam TV kwa kuwa mchezaji bora wa mechi hiyo. Simba SC sasa itapambana na KCC ya Uganda pia katika Fainali Jumatatu Saa 10:00 Uwanja wa Amaan. Ikumbukwe Simba na KCC zote zimetokea Kundi B na katika mechi baina yao, zilitoka sare ya bila kufungana. Kikosi cha Simba SC leo kilikuwa; Ivo Mapunda, Haruna Shamte, Issa Rashid ‘Baba Ubaya’/William Lucian 'Gallas', Joseph Owino, Donald Mosoti, Jonas Mkude, Haroun Chanongo, Amri Kiemba/Said Ndemla, Ramadhani Singano ‘Messi’, Amisi Tambwe/Ramadhani Chombo ‘Redondo’ na Awadh Juma/Uhuru Suleiman.  URA; Mugabi Yassin, Samuel Ssenkoom, Alan Munamba/James Kasibante, Mussa Doca, Jonathan Mugabi, Oscar Agaba, Augustine Nsumba, Owen Kasuule, Erisa Sekisambu/Ngama Emmanuel, Feni Ali/Milos Ilic na Hashimu Sempalia.

PICHA >kwa msaada wa binzubeiry blog 

Thursday, January 9, 2014

MESSI ARUDI APIGA MBILI NDANI YA DAKIKA MBILI

Mshambuliaji Lionel Messi kushoto usiku huu ametokea benchi na kufunga mabao mawili katika ushindi wa 4-0 wa Barcelona dhidi ya Getafe Uwanja wa Camp Nou katika mechi ya Kombe la Mfalme. Messi aliyekuwa majeruhi kwa muda mrefu, alifunga katika dakika za 89 na 90 baada ya Cesc Fabregas kutangulia kufunga katika dakika za nane na 62 kwa penalti.  

MANCITY HATARI TUPU YAPIGA MTU 6-0 CARPITAL ONE CUP NA KUNUSA HATUA YA AINALI

MANCHESTER City imeilaza mabao 6-0 Wes Ham United katika Nusu Fainali ya kwanza ya Kombe la Ligi England usiku huu Uwanja wa Etihad.
 
Alvaro Negredo amefunga mabao matatu katika dakika za 12, 26 na  49, kabla ya Yaya Toure kufunga dakika ya 40, Edin Dzeko mawili dakika za 60 na 89.
Sasa kocha Manuel Pellegrini na kikosi chake atakuwa kazi nyepesi katika mchezo wa marudano Uwanja wa Upton Park wiki mbii zijazo 
 

Tuesday, January 7, 2014

WALEZI WA SIMBA NA YANGA WAGAWA JEZI MPYA

KAMPUNI ya Bia Tanzania (TBL) kupitia bia yake Kilimanjaro Premium Lager imekabidhi vifaa vya michezo kwa timu za Simba na Yanga kwa ajili ya mzunguko wa pili wa Ligi Kuu itakayoanza Januari 25 mwaka huu. Kilimanjaro Premium Lager ni wadhamini wakuu wa klabu za Simba na Yanga na vifaa hivyo ni moja ya utekelezaji wa makubaliano ya mkataba baina ya pande mbili hizo.
Meneja wa Bia ya Kilimanjaro, George Kavishe (katikati) akiwa na Mkurugenzi wa Masoko wa Yanga, George Simba kulia na Ofisa Utawala wa Simba SC, Hussein Mozzy kushoto wakati wa makabidhiano hayo 
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Meneja wa bia ya Kilimanjaro George Kavishe alisema Simba na Yanga wamekuwa na ushirikiano mzuri kuhakikisha mdhamini anakuwa na furaha na kufurahia matunda ya udhamini huo. “Katika kuendeleza yale tuliyokubaliana katika mikataba yetu, tunawakabidhi vifaa hivi ikiwa ni maandalizi ya mzunguko wa pili wa Ligi Kuu ya Vodacom. “Lakini pia nitumie fursa hii kuwashukuru Mwenyekiti wa Simba Ismael Aden Rage pamoja na Mwenyekiti wa Yanga Yusuph Manji kwa ushirikiano wao katika kipindi cha uongozi wao. “Nichukue fursa hii kwa niaba ya TBL kuwatakia mzunguko mwema wa Ligi Kuu ya Vodacom pamoja,” alisema Kavishe. Kwa upande wake Afisa Tawala wa Simba Hussein Mozzy aliwashukuru wadhamini hao huku akisema timu yao imejiandaa vema na mzunguko wa ligi hiyo na kwa sasa ipo Zanzibar ikishiriki michuano ya Kombe la Mapinduzi. Kwa upande wake Mkurugenzi wa Masoko wa Yanga George Simba aliwashukru wadhamini hao Kilimanjaro Premium Lager kwa kuonyesha ushirikiano wao na kutimiza majukumu yao ya kimkataba. Vifaa vilivyogawiwa vyenye thmani ya zaidi ya Sh milioni 60 ni pamoja na jezi, mipira, viatu, mabegi, soksi na raba za mazoezi na vitu vingine.

AZAM MWENDO MDUNDO YAINYUKA ASHANTI BILA YA HURUMA

HATUA ya makundi ya Kombe la Mapinduzi imehitimishwa usiku huu kwa mchezo wa mwisho wa Kundi C, Azam FC ikiilaza Ashanti United bao 1-0 Uwanja wa Amaan, Zanzibar.
  Bao pekee la Azam leo limefungwa na Mganda, Brian Umony dakika ya 60, akiunganisha krosi ya Kipre Tchetche kutoka wingi ya kulia.
Kipre Tchetche akimpongeza Brian Umony baada ya kufunga leo Uwanja wa Amaan
Kwa matokeo hayo, Ashanti inayofundishwa na kocha mkongwe, Alhaj Abdallah Athumani Seif ‘King Kibaden’ inaaga mashindano haya. Ashanti ilihitaji sare tu katika mchezo wa leo ili ifuzu Robo Fainali, lakini imalambwa kidude.  
  Timu zilizofanikiwa kuingia Robo Fainali ni Azam FC na Tusker ya Kenya kutoka Kundi C, Simba SC na KCC ya Uganda kutoka Kundi B, URA ya Uganda, Chuoni, Cloves Stars na KMKM.
  Robo Fainali zitachezwa Jumatano, Tusker na URA Saa 8:00 mchana na Azam FC na Cloves Saa 10:00 jioni Uwanja wa Gombani Pemba na Uwanja wa Amaan, mechi ya kwanza itakuwa kati ya KCC na KMKM Saa 10:00 na Simba SC na Chuoni Saa 2:00 Usiku.


PICHA KWA MSAADA WA BINZUBEIRY BLOG

MAN UNITED YAHAMIA KWA DIEGO COSTA KWA HASIRA ZOTE

KLABU ya Manchester United imepiga hatua katika harakati zake za kusaka za kuimarisha kikosi chake baada ya kwenda kuwatazama Diego Costa na Ander Herrera mwishoni mwa wiki.
Baada ya kutolewa kwenye Kombe la FA na Swansea, kipigo ambacho ni mwendelezo wa msimu mbaya United, kocha David Moyes amesema kwamba kuna jitihada za dhati klabu hiyo ya Old Trafford kusajili wachezaji. 
Amekuwa akisaka beki wa kushoto, kiungo na mshambuliaji Ulaya mzima.
Mlengwa mkuu: Manchester United inataka kumsajili mshambuliaji wa Atletico Madrid, Diego Costa
Flying high: Diego Costa and Atletico hit the top of La Liga after beating Malaga 1-0
Diego Costa aliiwezesha Atletico kupanda kileleni mwa La Liga baada ya kuifunga Malaga 1-0

Msaka vipaji mkuu wa United, Robbie Cooke alimshuhudia mchezaji wa bei ghali Costa akicheza dakika zote 90 huku Atletico Madrid ikishinda 1-0 dhidi ya Malaga Jumamosi.
Koke – mchezaji ambaye United wamekuwa wakihusishwa naye lakini hawana nia ya kumsajili mwezi huu – alifunga bao pekee kwenymchezo huo.
Cooke alikuwa mmoja wa watu wa benchi la Ufundi walioambatana na Moyes kutua Old Trafford wakitokea Everton na mpango huo ulimfanya asafiri kutoka pwani ya kusini ya Hispania hadi kaskazini mwa San Sebastian, kumuangalia mchezaji wa Atletico Bilbao, Herrara akicheza mechi ya kipigo cha 2-0 kwa Real Sociedad.
Costa, ambaye pia alitakiwa na Liverpool Agosti mwaka jana na hivi karibuni amekuwa akihusishwa na kuhamia Chelsea na Arsenal, amekuwa mmoja wa washambuliaji gumzo Ulaya msimu huu, baada ya kufunga mabao 19 katika mechi 18 na kuisaidia timu yake kuwa mpinzani mkuu wa Barcelona katika mbio za ubingwa wa La Liga.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 25 aliyekataa ofa ya uraia wa Hispania mwaka jana ili aichezee Brazil katika Kombe la Dunia, nchi yake halisi aliyozaliwa, alisaini Mkataba mpya na Atletico ili kumzuia kwenda Liverpool, lakini anaweza kuuzwa kwa Pauni Milioni 31.

MASHETANI BADO YAZIDI KUMSUMBUA MOYES

Suala hapo lipo wazi sana ... Wenye upeo na wasiotekwa na mapenzi na timu iyo waliona tangu msimu uliopita ila wale walio wenzangu wenye mahaba niue wakaona timu yao inanguvu...

Msimu uliopita Manchester ilichukua taji, kwakua Rooney na van persie walikua wapo vizuri hasa van persie hakupata maumivu ya mara kwa mara ila kiujumla team iyo ilikua ya kawaida sana kwa wachezaji ambao ferguson Alikua ana watumia ...

Nakumbuka shafih dauda alisema iyo team ina mwili wa baunsa mbele ina forward kali ila kuanzia kwenye midfield ya chini na mabeki wake ni dhaifu .. Watu mkamtukana sana ...

Ferguson alilijua hilo suala kua kikosi chake anachotumia ni cha kawaida na sehemu ya defensive ya team iyo kuanzia kiungoni ni dhaifu alichokua anafanya ili kuficha madhaifu Alikua wakicheza mechi team yote anaiweka nyuma ili wasiruhusu goli huku wakitumia strikers zao wawili world class Rooney na van persie kuwapa matokeo , na Alikua akishapata ushindi Alikua hafunguki tena kushambulia .. Sio siri msimu ulipita united ilichukua ubingwa huku ikiwa inacheza mpira wa ovyo sana ila hamkuliona hilo kwakua mlikua mnapata ushindi ...

Huyu David Moyes amekuja na gundu kwanza kabisa Kuyumba kwa van persie kimajeruhi, na pili anatumia team ile ile ya Ferguson wachezaji wale wale ila tatizo lake yeye anataka kufunguka ashambulie muda wote Wakati wachezaji hana wa kufanya hivyo mwisho wa siku anaanza kufungwa yeye na kuanza kupata Shida ya kusawazisha, Ferguson mwenzake Alikua anaiweka team nyuma anaacha van persie na Rooney wafanye yao ila hakua anapandisha team yote kama moyes, Ferguson Alikua afungui uwanja hivi ....

Hiyo team hata haihitaji hata mabadiliko sana kuna wachezaji, humo humo ndani ya team wana hitaji kuaminiwa wapate nafasi za kucheza wanaweza kuleta utofauti, na pia David Moyes anasema hamna watu wa kuwasajili Wakati kuna kuna mafundi kibao tu wapo team za kawaida wanaoweza kuongeza kitu kipya kwenye team ... Kwa mfano Oscar wa Chelsea watu wamemsajili kutoka kwao brazil kaja kufanya mambo hata hakutoka kwenye team kubwa za ulaya ... Fernandinho wamemtoa shaktar donest team isiyoweza kuvumilia offer kutoka team kubwa.

Mimi nina sema Combination ya Rooney na van persie ni combination hatari zaid kuliko hata zlatan na cavan, negredo na aguero au suarez na sturridge ... ila Rooney na van persie msimu huu wanatumia muda mwingi kufanya kazi ya viungo wao kuliko kufunga magoli ....

Wilfred Zaha Mchezaji Bora Championship mara mbili mfululizo sidhani kama angeshindwa kucheza vizuri kama angeaminiwa, kwa sasa hivi anavyocheza mechi moja kwa miezi miwili ni kumfanya asijiamini uwanjani na kuogopa zaid kuharibu ....

Na pale wapo wengi tu kwenye janga hili, hawa akina Anderson na Kagawa hawaaminiwi kwenye mechi za kawaida wanakuja kupangwa kwenye mechi zilizo very trick alafu wakicheza ovyo wanasugua benchi muda mrefu ....

United itasimama tena kama wakiamua kusimama tena ila kama akiendelea kuwatumia wachezaji wale wale vipenzi vya Ferguson ataua iyo team kwakua yeye Moyes Sio Ferguson hawezi kuchimba matokeo ya ushindi kama hata team ikiwa mbovu...

KAKA ATIMIZA MABAO 100 MILAN

Leo hii kiungo wa AC MILAN raia wa Brazil Ricardo KAKA ameifungia timu yake mabao mawili kwenye ushindi wa mbao 3-0 dhidi ya ATALANTA kwenye mchezo wa Serie A. kaka kabla ya mchezo wa leo alikuwa ameifungia Milan mabao 99.

Sunday, January 5, 2014

TAKWIMU MBALIMBALI ZA MWAKA ULIOPITA


LEVANDOSKI AJIUNGA BAYERN MUNICH RASMI


Mshambuliaji wa Borussia Dortmund Robert Lewandowski atajiunga na klabu ya Bayern Munich kwa uhamisho huru mwishoni wa mwa msimu huu, mabingwa wa Ujerumani wametangaza.
           
Mshambuliaji huyo wa Poland, ambaye aliisadia Dortmund kushinda makombe mawili mfululizo ya Bundesliga 2011 na 2012, amesaini mkataba wa miaka mitano. 
Lewandowski alitangaza nia yake ya kuondoka Westfalenstadion pindi mkataba wake utakapomalizika mwishoni mwa msimu huu, na akawa anahusishwa na kujiunga na wapinzani wao Bayern. 
Lewandoski, 25, alijaribu kulazimisha kuuzwa kipindi cha kiangazi kilichopita lakini Dortmund waligoma kumuuza na kusisitiza lazima amalize mkataba wake.
Mwenyekiti wa Bayern Karl-Heinz Rummenigge alitangaza dili la Lewandoski, akisema: "Tuna furaha uhamisho huu umekamilika kwa mafanikio.
"Robert Lewandowski ni mmoja ya washambuliaji bora ulimwenguni, atakiongezea ubora kikosi chetu cha FC Bayern."

GWIJI LA SOKA NCHINI URENO AFARIKI DUNIA

GWIJI wa soka kutoka taifa la Ureno, Eusebio amefariki dunia, akiwa na umri wa miaka 71, baada ya kusumbuliwa na matatizo ya moyo kwa muda mrefu. Eusebio alizaliwa nchini Msumbiji kama Eusebio da Silva Ferreira na anatajwa kama mmoja wa wachezaji bora zaidi kuwahi kutokea duniani. Aliitumikia klabu ya mjini Lisbon,Benfica FC kwa miaka 22 ambapo uwezo wake wa mbio na kasi, kuutumia vyema mguu wake wa kulia na mbinu za kimpira kulimpa umaarufu sana nchini Ureno na kubatizwa jina la The Black Pearl or the Black Panther.
Pumzika kwa amani Eusebio
Wakati wa uchezaji wake alifunga mabao 733 katika mechi 745, pia alifunga mabao tisa kwenye michuano ya kombe la dunia ya mwaka 1966 na kuwa mfungaji bora wa mashindano hayo na kuisaidia Ureno kushika nafasi ya tatu kwenye michuano hiyo. Eusebio da Silva Ferreira alikuwa mfungaji bora wa fainali za Kombe la Dunia zilizofanyika nchini England mwaka 1966 kuanzia Julai 11, hadi Julai 30 wenyeji England wakiifunga Ujerumani Magharibi 4–2 na kutwaa Kombe. Eusebio alifunga mabao tisa na kuwapiku Helmut Haller mabao sita, Geoff Hurst, Franz Beckenbauer, Ferenc Bene na Valeriy Porkujan mabao manne kila mmoja na Luis Artime na Bobby Charlton waliofunga matatu kila mmoja.  Eusebio aliyezaliwa Januari 25, mwaka 1942, anachukuliwa kama mchezaji bora daima kuwahi kutokea duniani na Shiriksiho la Viwango la Kimataifa (IFFHS). Aliisaidia Ureno kushika nafasi ya tatu kwenye fainali hizo kwa mabao yake hayo, sita akifunga kwenye Uwanja wa Goodison Park na kuchaguliwa kuwa Mwanasoka Bora Ulaya mwaka 1965. Aliichezea Benfica kwa miaka 15 na ndiye mfungaji bora daima wa klabu hiyo.

Saturday, January 4, 2014

RATIBA: MICHEZO YA KOMBE LA FA NCHINI ENGLAND WIKI HII RAUNDI YA 3

 IN CENTRAL AFRICA TIME

Saturday 04 January 2014
Blackburn RoversvManchester CityEwood Park14:45
Kidderminster HarriersvPeterborough UnitedAggborough17:00
RochdalevLeeds UnitedSpotland17:00
Bristol CityvWatfordAshton Gate17:00
Southend UnitedvMillwallRoots Hall17:00
Ipswich TownvPreston North EndPortman Road17:00
EvertonvQueens Park RangersGoodison Park17:00
West Bromwich AlbionvCrystal PalaceThe Hawthorns17:00
MiddlesbroughvHull CityRiverside Stadium17:00
Norwich CityvFulhamCarrow Road17:00
Macclesfield TownvSheffield WednesdayThe Moss Rose Ground17:00
Port ValevPlymouth ArgyleVale Park17:00
BournemouthvBurton AlbionGoldsands Stadium17:00
BarnsleyvCoventry CitySixfields Stadium17:00
Newcastle UnitedvCardiff CitySt. James' Park17:00
SunderlandvCarlisle UnitedStadium of Light17:00
Doncaster RoversvStevenageThe Keepmoat Stadium17:00
Bolton WanderersvBlackpoolReebok Stadium17:00
Wigan AthleticvMK DonsDW Stadium17:00
Stoke CityvLeicester CityBritannia Stadium17:00
Grimsby TownvHuddersfield TownBlundell Park17:00
Yeovil TownvLeyton OrientHuish Park17:00
Aston VillavSheffield UnitedVilla Park17:00
Brighton and Hove AlbionvReadingAmex Stadium17:00
Charlton AthleticvOxford UnitedThe Valley17:00
SouthamptonvBurnleySt. Mary's Stadium17:00
ArsenalvTottenham HotspurEmirates Stadium19:15
Sunday 05 January 2014
Nottingham ForestvWest Ham UnitedCity Ground14:00
SunderlandvCarlisle UnitedStadium of Light16:00
Derby CountyvChelseaPride Park Stadium16:15
Port ValevPlymouth ArgyleVale Park17:00
LiverpoolvOldham AthleticAnfield17:00
Manchester UnitedvSwansea CityOld Trafford18:30
Wednesday 08 January 2014
Crawley TownvBristol RoversBroadfield Stadium21:45

MAKALA: MAN UNITED KUWA KAMA ARSENAL ILEEEEE


Na IZOBABRU
YALE mawazo ya wachambuzi wa soka kwamba Manchester United haitakuwa na ujanja mara baada ya kuondoka kwa Kocha Alex Chapman Ferguson, kwamba itayumba tu yameanza kutimia.


Kweli hilo limeonekana, Kocha David Moyes ndiye yuko ‘motoni’ kwa kipindi chote tokea ameingia, kikosi chake kimeanza kuonekana si ile Man United ya Ferguson na uhakika wa ushindi umeshuka hadi 56% wakati kipindi cha Ferguson ulikuwa hadi 82%.

Kipigo cha juzi cha mabao 2-1 kutoka kwa Tottenham Hotspur maana yake Man United imeanza mwaka mpya wa 2014 kwa kipigo, lakini kipigo hicho kimerudisha tena hofu.

Ushindi wa mechi tano mfululizo ulionyesha kurudisha matumaini kwa mashabiki wa Man United ambao walionekana kukata tamaa baada ya timu yao kupoteza mfululizo.

Mwenendo wa Man United unaonyesha mambo mawili, hofu ya kubeba ubingwa na tayari wadau wameanza kuindoa wakitumia historia, kwamba timu inapopoteza mechi tano katika Ligi Kuu England, basi nafasi ya kubeba ubingwa nayo inatoweka.

Hilo ni kundi la kwanza, kundi la pili ni lile linalofikiri utafikia wakati hata kupata zile nafasi nne za juu itakuwa kazi kwa kuwa sasa Man United iko katika nafasi ya saba ikiwa na 34, tofauti ya pointi 11 na vinara Arsenal 45.

Huenda majibu yakasubiri muda, lakini mechi sita zijazo za Man United zinaweza kuwa na majibu yote, kwamba kweli imebaki kwenye kuwania ubingwa, au itachukua nafasi ya Arsenal iliyoishika kwa zaidi ya miaka minne.

Arsenal imekuwa ikijulikana kwa kutokuwa na nafasi ya kutwaa ubingwa wa England ambao mara ya mwisho iliubeba msimu wa 2003/ 2004. Baada ya hapo imekuwa ikiushuhudia kwenye ‘kideo’ tu.
Sifa ya Arsenal wamekuwa na sifa ya kuwania nafasi nne za juu ili washiriki Ligi ya Mabingwa Ulaya na si ubingwa.

Utaona Man United ndiyo ilikuwa ikipewa nafasi kubwa ya kutwaa ubingwa, baadaye Chelsea halafu ikaibuka Man City ya Roberto Mancini na kweli ikafanya kweli.

Lakini msimu huu wanaopewa nafasi ya ubingwa ni Arsenal, Man City, Chelsea na Liverpool.

Kwa Man United, majibu ni baada ya mechi hizo sita, kwamba wamo kwenye ubingwa au nne bora kama enzi za Arsenal na wakiwemo, watamtoa nani.
Kipindi cha Januari 11 hadi Febrauri 12, Man United itakuwa na mechi sita, zikiwemo dhidiya Chelsea na Arsenal.

Januari 11, Man United itakuwa nyumbani kuwakaribisha Swansea ambao hawaaminiki. Halafu Januari 19 itafunga safari kwenda London kupambana na wabishi wa Mourinho, Chelsea.

Mechi nne zitakazofuatia ni dhidi ya Cardiff na Man United itakuwa imerejea nyumbani.Halafu itaianza Februari ugenini dhidi ya wababe Stoke City kabla ya kurudi nyumbani Februari 9, kuwakaribisha Fulham wanaokwenda kwa mwendo wa kusuasua.

Wakati majibu yanasubiriwa, mechi ya sita ndiyo kazi ngumu zaidi kwa kuwa Man United watakuwa wanakutana na Arsenal tena wakiwa ugenini Emirates.

Inawezekana majibu ya nafasi ya Man United kwenye ubingwa au kuwania kucheza Ulaya yatajulikana mapema au la, kutegemeana na inavyokwenda.

Lakini ndani ya mechi sita, kazi inaonekana ni ngumu kwa kuwa inakutana na timu mbili za juu na ngumu na zote itakuwa ugenini dhidi ya Chelsea na Arsenal.

Kama haitoshi, Man United itakuwa na wakati mgumu, pamoja na kwamba haiaminiki inapokuwa nyumbani kama ilivyokuwa awali, kati ya mechi hizo sita, nusu ni za ugenini zikiwemo hizo ngumu za jijini London.

Hivyo, ili iwe na uhakika, lazima ihakikishe mechi tatu za nyumbani dhidi ya Swansea, Cardiff na Fulham inatupia pointi tisa kibindoni.

TIMU MBILI LIGI KUU MALAWI ZAPIGWA FAINI

Vilabu viwili vya mpira wa miguu nchini Malawi vya Mighty Wanderers na Silver Strikers vimefungiwa kufuatia ghasia za mashabiki katika mchezo wao wa Desemba 28 mwaka jana.
Shabiki mmoja aliuawa na 20 kujeruhiwa katika uwanja wa Balaka, na mechi hiyo kufutwa.
Silver Strikers wamefungiwa kwa miezi minane na kutozwa dola za Kimarekani 6640.00, wakati ambapo timu ya Mighty Wanderers wamefungiwa kwa miezi mitano na kupigwa faini ya dola za Kimarekani 1620.00.

Timu hizo zinaweza kukata rufaa dhidi ya adhabu hiyo lakini zikiwa zimetoa kiasi cha dola $1046 katika muda wa saa 48 tangu kutolewa kwa adhabu hiyo.
Timu ya Mighty Wanderers ya Malawi


Kamati ya nidhamu ya ligi ya Malawi imezipata timu zote mbili kuwa na hatia kwa kushindwa kudhibiti vitendo vya mashabiki wao kinyume na kanuni za Fifa na hivyo kusababisha mchezo wa soka kuwa vurugu.
Silver Strikers nao walipatikana na hatia kwa kuchochea ghasia zilizosababisha kufutwa kwa mchezo huo, ukiwa katika dakika ya 61, wakati ambapo Mighty Wanderers FC ilishindwa kutoa ulinzi wa kutosha kwa timu ngeni ya Silver Strikers pamoja na watazamaji.
 Timu ya silva strikers ya malawi

Katika taarifa hiyo, Ligi ya Malawi, "Super League of Malawi" wamesema kuwa adhabu hizo zimekuwa kali kwa sababu timu hizo mbili zimekuwa zikijirudia kutenda makosa.
Chombo hicho pia kimeamuru timu zote mbili kurudia mchezo huo bila kuwa na watazamaji, kabla ya tarehe 4 Januari, adhabu zao zitakapoanza kutekelezwa.
Hata hivyo, Silver Strikers wameonyesha kuwa watacheza mchezo wa marudiano iwapo tu utaanzia pale ulipoishia, yaani dakika ya 61 wakati walipokuwa wakiongoza kwa bao 1-0.


YANGA WAANZA KAZI NA MAKOCHA WAPYA

Mabingwa watetezi wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara timu ya Young Africans leo imeeanza kujifua katika viwanja vya bora Mabatini Kijitonyama kujiandaa na mzunguko wa pili wa Ligi Kuu na mashindano ya kimataifa chini ya kocha msaidizi Charles Boniface Mkwasa. Young Africans ilisimama kufanya mazoezi kwa siku takribani tatu kufuatia kufanya mabadiliko ya benchi la Ufundi na leo rasmi imeanza mazoezi asubuhi chini ya makocha wasaidzi Mkwasa na kocha wa makipa Juma Pondamali.
Mkwasa alitumia muda wa dakika 5 kuongea na wachezaji wote waliofika mazoezini siku ya leo, kuwaelekeza nini wanapaswa kufanya na kuzingatia mafunzo yake ambapo wachezaji waliweze kutekeleza kwa kiwango cha hali ya juu.
Kocha wa makipa Juma Pondamali aliwafua vilivyo magolikipa Juma Kaseja, Ally Mustafa "Barthez" na Deogratias Munish "Dida" na kusema huu ni mwanzo tu kwani anaamini wachezaji hao watakua katika kiwango kizuri kutokana na uwezo wanaouonyesha katika mazoezi anayaowapatia.
Kikosi cha Young Africans kesho kitaendelea na mazoezi asubuhi katika uwanja wa Mabatini Kijitonyama ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya mzunguko wa pili na mashindano ya kimataifa. Aidha washambuliaji Hamis Kiiza na Emmanuel Okwi waliokwenda kwao nchini Uganda kwa ajili ya matatizo ya kifamilia wanatarajiwa kurejea nchini mwishoni mwa wiki tayari kuungana na wenzao kujiandaa na mzunguko wa pili.

TOM OLABA APATA SHAVU RUVU SHOOTING


MAAFANDE wa jeshi la kujenga Taifa wa mkoani Pwani, Ruvu Shooting, wamemsainisha mkataba wa miezi sita kocha, Tom  Alex Olaba ili kurithi mikoba ya kocha aliyetimkia Yanga, Charles Boniface Mkwasa `Masta`.

Afisa habari wa klabu hiyo, Masau Bwire amesema Olaba ameshafika Mabatini jioni ya leo na kila kitu kimemalizika baina ya pande mbili.

“Tunafurahi kutangaza kuwa tumempata mrithi wa Mkwasa. Olaba ni mwalimu mzuri na tuna uhakika atatuongoza vizuri mzunguko wa pili”. Alisema Masau.

Olaba ambaye amewahi kuifundisha Mtibwa Sugar ataanza kazi rasmi kesho kukinoa kikosi cha Ruvu Shooting kuelekea mzunguko wa pili wa ligi kuu soka Tanzania bara unaotarajia kuanza kutimu vumbi januari 25 mwaka huu.

Kwa upande wake Olaba alisema amefurahi kurudi ligi kuu Tanzania bara kwa mara nyingine, lakini hawezi kuzungumza lolote mpaka atakapoongea na wachezaji wake hapo kesho mazoezini.

“Nimechoka sana ndugu yangu, ujue nimetoka safarini. Hata hivyo kwasasa siwezi kuzungumza lolote mpakaa nikikutana na kuongea na wachezaji wangu. Kikubwa nimefurahi kurudi  katika changamoto ya ligi ya Tanzania”, Alisema Olaba.

SIMBA YALAZIMISHWA SARE JANA DHIDI YA KCC YA UGANDA

SIMBA SC imegawana pointi na KCC ya Uganda baada ya sare ya bila kufungana katika mchezo wa Kundi B, Kombe la Mapinduzi usiku huu Uwanja wa Amaan, Zanzibar.
  Kwa ujumla timu zote zilitoshana nguvu na maarifa kwa dakika zote 90 za mchezo huo, huku makipa wote, Ivo Mapunda wa Simba na Magoola Omar wa KCC 
wakistahili sifa kwa kuokoa michomo mingi ya hatari. Mabeki wa KCC walimdhibiti vizuri winga machachari wa Simba SC, Ramadhani Yahya Singano ‘Messi’ leo, wakati pia beki Mkenya, Donald Mosoti Omwanwa aliiongoza vyema safu ya ulinzi ya Simba SC. 
Kipa wa KCC, Magoola Omar akiruka juu kupangua mpira kichwani kwa mshambuliaji wa Simba, Betram Mombeki jioni hii Uwanja wa Amaan
Matokeo hayo yanazifanya Simba SC na KCC ziendelee kukabana kileleni, kila timu ikiwa na pointi nne baada ya kucheza mechi mbili. Mapema jioni katika mchezo wa kwanza wa kundi hilo, wenyeji KMKM nao walitoshana nguvu na AFC Leopard ya Kenya kwa sare ya 0-0 pia. Mechi za Kundi B zitahitimishwa Januari 5, kwa Simba kumenyana na KMKM na KCC na Leopard. Michuano hiyo itaendelea kesho kwa mechi za Kundi C, Ashanti ikimenyana na Spice Stars na Azam FC na Tusker ya Kenya Uwanja wa Amaan, wakati Uwanja wa Gombani, Pemba Clove Stars itamenyana na URA ya Uganda na Mbeya City na Chuoni.
  Katika mchezo wa leo, kikosi cha Simba SC kilikuwa; Ivo Mapunda, Haruna Shamte, Issa Rashid ‘Baba Ubaya’, Donald Mosoti, Joseph Owino, Jonas Mkude, 

Ramadhani Singano/Zahor Pazi dk89, Amri Kiemba/Said Ndemla dk50, Amisi Tambwe/Betram Mombeki dk67, Uhuru Suleiman/Ramadhani Chombo dk48 na Haroun Chanongo/Edward Christopher dk78. 
  KCC; Magoola Omar, Saki Mpima, Kavuma Habibu, Kawooya Fahad, Kiiza Ibrahim, Senkumba Hakim, Waswa Herman, Masiko Tom, Tony Odur, Stephen Bengo/Gadafi Kiwanuka dk 58 na Wadri William. 

picha kwa msaada wa Binzubeiry blog

Friday, January 3, 2014

OLE GUNNAR SOLSKJAER KUINOA CARDIFF CITY RASMI

 Klabu ya Cardiff City imemtangaza rasmi mshambuliaji wa zamani wa Manchester Utd Ole Gunnar Solskjaer kuwa meneja wao mpya.
Solskjaer ambaye ni raia wa Norway hapo awali alikuwa kocha wa timu ya Molde aliyoiongoza kutwaa mataji mawili ya ligi kuu ya Norway.

MKWASA PONDAMALI KUINOA YANGA

 Uongozi wa Young Africans SC umepata warithi wa nafasi tatu za benchi la ufundi (Charles Boniface Mkwasa, Juma Pondamali na Dr. Suphian Juma), huku wakiendelea na mchakato kumpata kocha mkuu ambaye atachukua nafasi ya mholanzi Ernie Brandts aliyesitishiwa mkataba wake mwishoni mwa mwaka 2013. Charles Boniface Mkwasa "Master" aliyekua kocha mkuu wa timu ya Ruvu Shooting katika mzunguko wa kwanza anachukua nafasi ya aliyekua kocha msaidizi Fred Felix "Minziro" ambaye muda wake umemalizika mwishoni mwa mwaka 2013. Mkwasa ambaye aliichezea Young Africans miaka ya 80's kwa kiwango cha hali juu pia alishawahi kuwa Kocha Mkuu/Msaidizi kwa kikosi cha Jangwani kwa vipindi tofauti jambo ambalo linamfanya aiwe mgeni katika mitaa ya Twiga na Jangwani.
Kocha wa makipa wa timu ya Taifa Tanzania "Taifa Stars" Juma Pondamali "Mensah" anachukua nafasi ya aliyekua kocha wa makipa mkenya Razaki Siwa ambaye pia alistishiwa mkataba wake mwishoni mwa mwaka 2013.
Pondamali golikipa aliyeichezea Yanga miaka ya 80's kwa kwa kiwango cha hali ya juu hata kufikia kuwa katika kikosi cha Tanzania kilichoshiriki mashindano ya Mataifa Afrika nchini Nigeria mwaka 1980, sio mgeni katika timu ya Young Africans kwani awali alishwahi kuwa kocha msaidizi kwa vipindi tofauti. Dr Suphian Juma anachukua nafasi ya Dr Nassoro Matuzya ambaye pia alisitishiwa ajira yake mwishoni mwa mwaka 2013 pamoja benchi la Ufundi.
Mara baada ya kuwapata viongozi hao watatu wa Benchi la Ufundi kikosi cha Young Africans kesho kitaanza mazoezi jioni katika Uwanja wa Bora Kijitonyama kujiandaa na mzunguko wa pili wa Ligi Kuu ya Vodacom pamoja na mashindano ya Kimataifa huku kocha Mkwasa akiongoza benchi hilo la Ufundi mpaka atakapopatikana kocha mkuu ambaye watafanya watafanya kazi kwa pamoja.

HATIMAYE KIUNGO TOM HUDDLESTONE ANYOA NYWELE ZAKE

Kiungo wa Hull City Tom Huddlestone ametimiza ahadi yake ya kunyoa nywele zake iwapo angefunga bao baada kukaa miaka miwili na nusu bila kufunga,kiungo huyo aliifungia timu yake bao moja kwenye mchezo ambao timu yake iliifunga Fulham mabao 6-0.