Tuesday, December 31, 2013

MESSI AWEKWA KITIMOTO SIMBA

KIUNGO nyota wa Simba SC, Ramadhani Yahay Singano ‘Messi’ leo asubuhi aliwekwa kikao cha dharula na viongozi wa klabu yake, kwa kuonyesha kitendo cha utovu wa nidhamu wakati wa safari ya timu hiyo visiwani Zanziabr kwenye Kombe la Mapinduzi.
  Wachezaji wa Simba SC wakiwa bandari ndogo ya Azam Marine, Dar es Salaam asubuhi tayari kwa safari ya Zanzibar, Messi alifika akiwa hana jezi ambayo wachezaji waliagizwa wavae wakati wa safari.
 
Kitendo hicho kiliwaudhi Wajumbe wa Kamati ya Utendaji ya Simba SC waliokuwa wanaongoza msafara, Ibrahim Masoud ‘Maestro’ na Said Pamba ambao walilazimika kumuita pembeni mchezaji huyo kumuhoji.
Baada ya utetezi wake, ilibidi na Meneja wa timu, Mganda Moses Basena aitwe kutoa ushahidi. Hata hivyo, Basena alionekana kutokubaliana na maelezo ya Messi, lakini viongozi wakaachana naye aendelee na safari.
 
Messi amekuwa kipenzi cha wana Simba SC tangu Desemba 21, mwaka huu acheze kwa kiwango cha juu katika mchezo dhidi ya mahasimu, Yanga wa Nani Mtani Jembe na kusaidia ushindi wa mabao 3-1.
 
Inaonekana kama sifa alizozipata baada ya mchezo huo, zinaanza kumfanya ajione yuko tofauti na wachezaji na wenzake, jambo ambalo viongozi wa klabu hiyo wanaonekana mapema kuanza kupambana nalo.

RATIBA:MICHEZO YA KESHO LIGI KUU ENGLAND 01 JAN 2014

Wednesday 01 January 2014
Swansea CityvManchester CityLiberty Stadium14:45
ArsenalvCardiff CityEmirates Stadium17:00
Crystal PalacevNorwich CitySelhurst Park17:00
FulhamvWest Ham UnitedCraven Cottage17:00
LiverpoolvHull CityAnfield17:00
SouthamptonvChelseaSt. Mary's Stadium17:00
Stoke CityvEvertonBritannia Stadium17:00
SunderlandvAston VillaStadium of Light17:00
West Bromwich AlbionvNewcastle UnitedThe Hawthorns17:00
Manchester UnitedvTottenham HotspurOld Trafford19:30

Thursday, December 26, 2013

MAN UNITED YASAKA SAINI YA MARCO REUS

KLABU ya Manchester United imeonywa kwamba mchezaji chaguo la kwanza la David Moyes katika usajili wa dirisha dogo, Marco Reus atawagharimu hadi Pauni Milioni 40 ili kumpata. 
Kiungo Reus ana thamani ya Pauni Milioni 29.4 Borussia Dortmund.
Lakini inafahamika mambo yamebadilika tangu Bayern Munich ionyeshe nia ya kutaka kumsajili Mario Gotze.
Itakugharimu! Borussia Dortmund inataka dau la Pauni Milioni 40 ili kumuuza Marco Reus, ambaye anatakiwa na Manchester United katika usajili wa Januari
World class: United would have to break their transfer record to sign the talented Reus, whom manager David Moyes has identified as a key target to galvanise their midfield
Kiwango cha dunia: United itavunja rekodi ya dau la usajili kumsajili mchezaji mwenye kipaji, Reus, ambaye kocha David Moyes amemtambulisha kama chaguo la kwanza katika wachezaji anaowataka

Mabingwa hao wa Ligi Kuu ya England watatakiwa kuvunja rekodi yao ya dau la usajili ili kuipata saini ya kiungo huyo mwenye umri wa miaka 24.
Wasaka vipaji wa United wakuwa wakisaka mchezaji wa kiwango cha dunia kwa nafasi yoyote. 
Pamoja na hayo, kiungo huyo anabakia kuwa chaguo lao la kwanza, ingawa pia wanasaka na washambuliaji, beki wa kushoto na beki wa kati waje kuwa warithi wa Patrice Evra na Rio Ferdinand mwishoni mwa msimu.
Nearing the end? United have started the search for Patrice Evra's replacement
Anaelekea mwisho? United imeanza kusaka mbadala wa Patrice Evra

MOHAMMEDI MATUMLA AMCHAKAZA NASSIB RAMADHANI

Bondia Mohamed Matumla kushoto akimwadhibu Nassibu Ramadhani wakati wa mpambano wao wa raundi kumi uliofanyika siku ya sikukuu ya krismas na kugombania pikipiki yenye thamani ya shilingi milioni 1.9 Matumla alishinda kwa pointi mpambano huo na kuibuka na bodaboda picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com
Bondia Mohamed Matumla kushoto akipambana na Nassibu Ramadhani wakati wa mpambano wao  uliofanyika siku ya sikukuu ya krismas na kugombania pikipiki yenye thamani ya shilingi milioni 1.9 Matumla alishinda kwa pointi mpambano huo na kuibuka na bodaboda picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com
Bondia Lulu Kayage kushoto akipambana na Mariam Abdallah wakati wa mpambano wao wa kusherehekea sikukuu ya krismas kayage alishinda kwa k,o picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com


lulu akinyooshwa mkono juu baada ya kushinda


l
Bondia Lulu Kayage kushoto akipambana na Mariam Abdallah wakati wa mpambano wao wa kusherehekea sikukuu ya krismas kayage alishinda kwa k,o picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com
Bondia Hamis Ajari kushoto akipambana na Cosmas Cheka wakati wa mpambano wao uriofanyika wakati wa sikukuu ya krismas cheka alishinda kwa point picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com


Bondia Sadiq Abdulazizi kushoto akipambana na Juma Fundi wakati wa mpambano wao uliofanyika wakati wa sikukuu ya krismas juma fundi alishinda kwa point mpambano uho picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com
Baadhi ya mashabiki waliouhulia mpambano huo uliokuwa mkali na kutoa burudani ya aina yake kwa mashabiki nchin

KISAKA AFARIKI DUNIA

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limepokea kwa masikitiko kifo cha aliyekuwa kocha wa makipa wa Simba, James Kisaka (57) kilichotokea leo asubuhi (Desemba 25 mwaka huu) katika Hospitali ya Burhani, Dar es Salaam.

Msiba huo ni mkubwa katika familia ya mpira wa miguu kwani Kisaka kabla ya kuwa kocha alikuwa mchezaji katika nafasi ya kipa. Mbali ya Simba, timu nyingine alizowahi kudakia ni Ndovu ya Arusha, Volcano ya Kenya na Small Simba ya Zanzibar.

Akiwa mwanafunzi Shule ya Sekondari Tambaza jijini Dar es Salaam aliwahi kuchezea timu za Oysterbay Stars, Eleven Stars ya Msasani, Sigara wakati ikicheza Ligi ya Temeke na Nyota Nyekundu kabla ya kutua Simba.

Pia alikuwemo kwenye timu ya Taifa ya vijana iliyokwenda Zimbabwe kwenye sherehe za uhuru wan chi hiyo mwaka 1980. Vilevile alikuwa mmoja wa wachezaji waliounda kombaini ya Tanzania ya UMISSETA akiwa na akina Said George, Nico Njohole, George Kulagwa na wengine. Hivyo mchango wake katika mchezo huu tutaukumbuka daima.

Kwa mujibu wa kaka wa marehemu, Benny Kisaka, James alikuwa akisumbuliwa na ugonjwa wa miguu kufa ganzi na matatizo ya kutoona vizuri.

Msiba uko nyumbani kwake Mbezi Mwisho (Kwa Yusuf), na anatarajia kuzikwa nyumbani kwao Kijiji cha Lusanga, Muheza mkoani Tanga.

TFF tunatoa pole kwa familia ya marehemu Kisaka, klabu ya Simba na Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) na kuwataka kuwa na subira na uvumilivu katika kipindi hiki kigumu cha msiba huo mzito.

Marehemu Kisaka ameacha mjane na watoto wanne. Bwana alitoa, Bwana ametwaa. Jina lake lihimidiwe.

Tuesday, December 24, 2013

FELLAINI AFANYIWA PASUAJI WA MKONO

Mcheza kiungo wa Manchester United Marouane Fellaini huenda asicheza mechi yoyote kwa muda wa wiki sita zijazo baada ya kufanyiwa upasuaji wa mkono.

Fellaini, 26, amekuwa akiuguza jeraha la mgongo na wasimamizi wa Manchester United wakaamua mchezaji huyo ambaye pia alikuwa na jeraha lingine, afanyiwa upasuaji wa mkono kwanza.

Fellaini amekuwa na tatizo hilo la mkono tangu alipojeruhiwa wakati wa mechi yao ya kuwania kombe la klabu bingwa barani ulaya dhidi ya Shakhtar Donetsk Oktoba mwaka huu.

Fellaini alipata jeraha lingine la mgongo wakati wa mechi ya ligi kuu dhidi ya Everton tarehe nne Desemba.
Moyes ambaye alimsajili mchezaji huyo kwa kitita cha pauni milioni 27.5 Septemba mwaka huu, amesema kuwa tatizo hilo la mgongo huenda likachukua muda mrefu zaidi.

MOHAMMEDI MATUMLA NA RAMADHANI NASSIBU KUKIPIGA XRISMAS

Bondia Mohamed Matumla kushoto na Nassibu Ramadhani wakitunishiana misuli baada ya kupima uzito kwa ajili ya mpambano wao leo katika

ukumbi wa friends corner hotel manzese Dar es salaam leo katikati ni promota wa mpambano huo kaike siraju Picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com


Promota kaike Siraju akiwainua juu mikono Bondia Mohamed Matumla kushoto na Nassibu Ramadhani kwa ajili ya mpambano wao wa kugombea pikipiki siku ya sikukuu ya Xmasi Picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com

PICHA:KIKOSI CHOTE CHA AZAMTV CHAENDA ZANZIBAR KURUSHA MICHUANO YA MAPINDUZI

 










Monday, December 23, 2013

RATIBA: MICHEZO YA LIGI KUU SIKU YA BOXING DAY NA MWISHO WA MWAKA HUU DECEMBER 29 2013

IN CENTRAL AFRICA TIME(CAT)

Thursday 26 December 2013
Hull CityvManchester UnitedThe KC Stadium14:45
Aston VillavCrystal PalaceVilla Park17:00
Cardiff CityvSouthamptonCardiff City Stadium17:00
ChelseavSwansea CityStamford Bridge17:00
EvertonvSunderlandGoodison Park17:00
Newcastle UnitedvStoke CitySt. James' Park17:00
Norwich CityvFulhamCarrow Road17:00
Tottenham HotspurvWest Bromwich AlbionWhite Hart Lane17:00
West Ham UnitedvArsenalBoleyn Ground17:00
Manchester CityvLiverpoolEtihad Stadium19:30
Saturday 28 December 2013
West Ham UnitedvWest Bromwich AlbionBoleyn Ground14:45
Aston VillavSwansea CityVilla Park17:00
Hull CityvFulhamThe KC Stadium17:00
Manchester CityvCrystal PalaceEtihad Stadium17:00
Norwich CityvManchester UnitedCarrow Road17:00
Cardiff CityvSunderlandCardiff City Stadium19:30
Sunday 29 December 2013
EvertonvSouthamptonGoodison Park15:30
Newcastle UnitedvArsenalSt. James' Park15:30
ChelseavLiverpoolStamford Bridge18:00
Tottenham HotspurvStoke CityWhite Hart Lane18:00

PICHA:MOYES NA WACHEZAJI WAKE WAFANYA ZIARA KWENYE MGAHAWA WA FERDINAND

MOYES AKIWASILI...
 Darren Fletcher AKIINGIA NA MCHUCHU

CHICHARITO NAYE NA MBEBE WA NGUVUU


BABU GIGGS...EEEH

KIUNGO Tom Cleverley NA MCHUCHU WAKE AKIWA NA RED, VIBEGA NJE..


KIPA NAMBA BEE WA UNITED,  Anders Lindegaard AKIWA NA MCHUCHU NDANI YA FULL BLACK

BABU NEVILLE NAYE WAMO

ROONEY NDANI YA NYUMBA NA COLEEN

VIDIC NA MTOTO WA POZI

CAPTAIN MSAIDIZI EVRA...

HUYU NI MBEBE WA DOGO CHRIS SMALLING, EEII!!

KITU CHA VAN PERSIE, MUITE BOUCHRA..CHINI MWENYEWE KWA POZIII

MPUTU AMUACHIA MIKOBA SAMATA TP MAZEMBE YEYE ATIMKIA ANGOLA


Mchezaji nyota zaidi wa TP Mazembe, Trésor Mputu ameondoka katika klabu hiyo na kutua nchini Angolan kuichezea Kabuscorp.
 Radio Okapi ya DR Congo imetangaza leo mchana kwamba Mputu amejiunga na klabu hiyo kwa kitita cha euro milioni 2 ambayo ni rekodi ya usajili na atakuwa akilipwa kitita cha euro 40,000 kwa mwezi.
Kuondoka kwa Mputu TP Mazembe, maana yake tegemeo anakuwa Mtanzania, Mbwana Ally Samatta ambaye amekuwa kipenzi kikubwa cha mashabiki wa timu hiyo baada ya Mputu.
Lakini mtandao wa TP Mazembe haukuthibitisha lolote kuhusu hilo na taarifa yake ya mwisho iliyotundikwa mtandaoni juzi imesema:  “Kutokana na taarifa za mitandao mingi kuwa Mputu anakwenda Angola, ukweli bado kila kitu hakijawa wazi na kama kuna ofa klabu inazisubiri kwa hamu kubwa:”
Mputu hakuonekana kambini baada ya Kocha Santos Mutubile kuita wacheza wa timu ya taifa ya DRC maarufu kama Leopards kujiandaa na michuano ya Kombe la Mataifa Afrika mwaka.
Lakini baadaye ilielezwa alisafiri kutoka Kinshasa hadi Luanda, Angola na kupokelewa na mashabiki kibao wa Kabuscorp kwenye uwanja wa ndege na baadaye akasaini mkataba wa mwaka mmoja.

BREAKING NEWZ: LUNYAMILA MAHUTUTI MWAANYAMALA


WINGA wa zamani wa Yanga na Taifa Stars, Edibily Lunyamila leo hii asubuhi amekimbizwa katika hospitali ya Mwananyamala baada ya kusumbuliwa na kifua na sasa anapumua kwa msaada wa mashine.

Mtandao huu ulifanikiwa kufika hospitalini hapo muda mfupi baada ya winga huyo kukimbizwa hospitalini hapo baada ya kuzidiwa tangu jana usiku akiwa nyumbani kwake Mbezi jijini Dar es Salaam.
Milandu sports imemshuhudia Lunyamila akiwa amelala kitandani katika wodi ya wanaume namba namba 5 kitanda namba 16 katika hospitali hiyo ya rufaa ya Kinondoni.

Daktari Madirisha Pascal anayemuhudumia winga huyo wa zamani, Lunyamila anasumbuliwa na tatizo la kifua ambalo linamfanya ashindwe kupumua vizuri.

“Kama mnavyomuona anapumua kwa msaada wa mashine na bado tunaendelea kumfanyia uchunguzi ili kubaini nini kinachomsumbua zaidi,” alisema Pascal.

Mmoja wa ndugu wa Lunyamila, Lameck John alisema kwamba, mchezaji huyo wa zamani alianza kujisikia vibaya jana Jumapili na leo asubuhi hali yake ilibadilika ndipo walipomkimbiza hospitali.

“Alianza kulalamika hawezi kupumua na kifua kinamsumbua pia mbavu zilikuwa zikimuuma, baada ya majibu ya vipimo tutajua kinachomsumbua zaidi,” alisema Lameck.

Kutokana na hali iliyoonekana hospitalini hapo, Lunyamila anahitaji huduma ya haraka ili kuweza kuokoa uhai wake kwani anapumulia mashine akiwa katika sehemu yenye joto kali hivyo anapambana na vitu vingi kwa wakati mmoja...

Taarifa za kiuchunguzi zilizofanywa na mwandishi wetu zimebaini Lunyamila anasumbuliwa na ugonjwa wa moyo.

 
''Nilikuja jana hospitali ya mwananyaala ikagundulika moyo wangu umekuwa mkubwa,hivi sasa naenda muhimbili kwa ajili ya vipimo zaidi nikifika na kukutana na daktari nitakujulisha ''
ilipofika mchana wa leo mwandishi alipokea simu kutoka kwa Lunyamila akimwambia ameambiwa arejee tena hospitali ya Mwananyamala.

SIMBA WAMBWAGISHA MANYANGA KOCHA WA YANGA , HATIMAYE ATIMULIWA RASMI LEO

RASMI Yanga SC imetangaza kuachana na kocha Mholanzi, Ernie Brandts siku mbili baada ya kufungwa mabao 3-1 na wapinzani wao wa jadi, Simba SC juzi katika mechi ya Nani Mtani Jembe Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Mwenyekiti wa Kamati ya Mashindano ya Yanga, Abdallah Ahmed Bin Kleb amewaambia Waandishi wa Habari leo asubuhi makao makuu ya klabu, Jangwani mjini Dar es Salaam kwamba Brandts amepewa notisi ya mwezi mmoja kwa mujibu wa taratibu za ajira na baada ya hapo ataondoka.
Bin Kleb amesema sababu za kumuondoa kocha huyo ni kushuka kwa kiwango cha timu katika siku za karibuni na haijatokana na kipigo cha juzi pekee.
“Kweli mwanzoni alipandisha kiwango cha timu, kilipanda sana, lakini baadaye kiwango kikaanza kushuka, tukasema tumpe muda kidogo, lakini tunaona mambo yanazidi kuharibika, hivyo tumeamua kuachana naye,”alisema.

Kuhusu Wajumbe wengine wa benchi la Ufundi, Bin Kleb alisema kwamba taratibu nyingine zinafuata na wakati huo huo klabu inasaka mwalimu mwingine atakayerithi mikoba ya Brandts.

Aidha, Bin Kleb amethibitisha ushiriki wa Yanga katika Kombe la Mapinduzi Januari mwakani visiwani Zanzibar na pia timu itafanya ziara ya Ulaya baada ya michuano hiyo.  

Pamoja na hayo, Bin Kleb amesema hawezi kuwapongeza watani wao Simba SC kwa kuwafunga 3-1, kwa sababu siku hiyo Yanga ilicheza mpira mbovu na ingeweza kufungwa hata timu inayoshuka daraja.

Sunday, December 22, 2013

PICHA: YANGA ALIPO LAMBISHWA BAO 3-1 JANA

 Wachezaji wa Simba na Yanga wakisalimiana.
 Kikosi cha Simba.
 Kikosi cha Yanga.
 Benchi la ufundi la timu ya Simba.
Benchi la Ufundi la Yanga.
 Henry Joseph wa Simba (kushoto) akichuana na beki wa Yanga, David Luhende.
 Henry Joseph wa Simba (kushoto) akichuana na beki wa Yanga, David Luhende.
 Mashabiki wa Simba wakishangilia bao la kwanza la timu yao.
 Raha ya ushindi.
 Furaha kwa Simba.

 Hamisi Kiiza akitafuta mbinu za kumtoka, Ramadhani singano.
 Ivo Mapunda akiruka juu kuokoa moja ya hatari langoni mwake.
 Mashabiki wa Yanga wakiwa hawaamini kilichotokea uwanjani baada ya kuchapwa 3-1 na watani zao wa jadi Simba.
 Juma Kaseja akibembelezwa na Mbuyu Twite baada ya kusababisha 
 Mmoja wa mashabiki wa Yanga akitolewa nje baada ya kuzimia uwanjani.
 Emmanuel Okwi akimtoka beki wa Simba.
 Wachezaji wa akiba wa Simba  wakishangilia baada ya filimbi ya mwisho. 
 Kocha wa Simba, Zdravko Logarusic akishangilia baada ya timu yake kuibuka na ushindi wa 3-1.
 Wachezaji wa Simba wakimnyanyua juu kocha wao, Zdravko Logarusic mara baada ya kumalizika kwa mchezo maalumu wa Nani Mtani Jembe uliofanyika kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. Simba ilishinda 3-1.




 Waziri wa Sheria na Katiba, Mathias Chikawe akimkabidhi kombe nahodha wa Simba Haruna Shamte.