Sunday, November 24, 2013

TP MAZEMBE YAPOTEZA FAINALI YA KWANZA YACHAPWA 2-0 TUNISIA

TIMU ya soka ya CS Sfaxien ya Tunisia, Jana imeutumia vyema Uwanja wa nyumbani, Stade Olympique de Rades baada ya kuilaza mabao 2-0  Tout Puissant Mazembe ya DRC katika Fainali ya kwanza ya Kombe la Shirikisho Afrika mjini Tunis.

Shukrani kwao, washambuliaji wa kimataifa wa Gabon, Ibrahim Didier Ndong aliyefunga bao la kwanza dakika ya 16 na mshambuliaji wa Taha Yassine Khenissi aliyefunga la pili dakika ya 90 na ushei wakimtungua kipa mahiri, Robert Muteba Kidiaba.

 Washambuliaji wote wa Tanzania, Mbwana Ally Samatta na Thomas Emanuel Ulimwengu walianza katika kikosi cha Mazembe pamoja na Tressor Mputu Mabi, lakini hawakuweza kuwanusuru mabingwa mara nne Afrika na kipigo hicho.Sfaxien, timu pekee iliyoshinda Kombe la Shirikisho mara mbili tangu kutambulishwa kwa mfumo mpya mwaka 2004, yenye maskani yake katika mji uliozungukwa na bahari ya Mediterranean, Sfax sasa itahitaji sare katika mchezo wa marudiano Novemba 30 au kufungwa kwa tofauti isiyozidi bao 1-0, mjini Lubumbashi ili kujinyakulia taji na kitita cha dola za Kimarekani, 625 000. Mshindi wa pili atapata dola 432 000. 

Mshindi pia atamenyana na mabingwa wa Ligi ya Mabingwa, Al Ahly ya Misri kuwania taji la Super Cup mechi itakayopigwa nchini Misri Februari 2014.

No comments:

Post a Comment