Friday, April 22, 2016

YANGA YATUPWA HUKU KWENYE MICHUANO YA SHIRIKISHO AFRIKA CAF..


CAF-cover
Kufuatia kuondoshwa kwenye michuano ya klabu bingwa barani Afrika hatua ya 16 bora, klabu ya Yanga imeangukia kwenye michuano ya kombe la Shirikisho Afrika. Kwa mujibu wa kanuni za CAF, vilabu vyote vinavyotupwa nje ya mashindano ya klabu bingwa Afrika vinakutana na washindi wa hatua ya 16 bora ya kombe la shirikisho kukipiga mchezo wa playoff unaoamua timu gani inasonga mbele kwenye hatua ya makundi katika kombe la shirikisho.

Usiku wa Jumatano Yanga ilisukumwa nje ya kombe la mabingwa Afrika na klabu ya Al Ahly ya Misri kwa kufungwa magoli 2-1 ugenini hivyo kuenguliwa kwenye michuano hiyo kwa jumla ya magoli 3-2 baada timu hizo kutoka sare ya kufungana goli 1-1 kwenye mchezo wa kwanza uliochezwa Dar.

April 21 imechezeshwa droo ya kuamua ni timu gani zitakutana kwenye mechi za mchujo zitakazoamua ni timu gani zitafuzu hatua ya makundi ya kombe la shirikisho Afrika.

Mabingwa watetezi wa VPL Yanga wamepangwa kucheza na klabu ya Sagrada Esparanca ya Angola ambapo Yanga wataanzia nyumbani mchezo wa kwanza (uwanja wa taifa, Tanzania) kati ya May 6-8 huku mchezo wa marudiano ukipangwa kufanyika Angola kati ya May 17-18, 2016.

RATIBA KAMILI.
Yanga-Angola

No comments:

Post a Comment