Thursday, October 24, 2013

PUYOL: NIPO KAMILI KUIKABILI REAL MADRID JUMAMOSI

Beki wa kimataifa wa Hispania na timu ya Barcelona y nchini humo Cariles Puyol  amedai kwamba yu tayari kuwa kabili mahasimu wao wa soka nchini humo Real Madrid jumamosi katika mchezo wa ligi kuu nchini humo.

Mechi hiyo maarufu kama El-Classico ambayo hukutanisha miamba hiyo huwa ya ushindani pale zinapokutana timu hizo katika ligi mbalimbali.

Nahodha huyo anataka kurudi uwanjani dhidi ya mahasimu wao hao ili kuja kuimarisha safu ya ulizi kutokana na ukali wa safu ya ushambuliaji kuwa hatari kwa wapinzani wao ikiongozwa na nyota wa dunia Cristiano Ronaldo.

Puyol alikuwa nje kwa kipindi kirefu sasa akiyatibu majeraha takribani miezi saba na anatarajiwa kuvaa jezi ya Barcelona na kuvaa kitambaa chake cha unahodha dhidi ya mahasimu wao.

No comments:

Post a Comment