Tuesday, January 7, 2014

MAN UNITED YAHAMIA KWA DIEGO COSTA KWA HASIRA ZOTE

KLABU ya Manchester United imepiga hatua katika harakati zake za kusaka za kuimarisha kikosi chake baada ya kwenda kuwatazama Diego Costa na Ander Herrera mwishoni mwa wiki.
Baada ya kutolewa kwenye Kombe la FA na Swansea, kipigo ambacho ni mwendelezo wa msimu mbaya United, kocha David Moyes amesema kwamba kuna jitihada za dhati klabu hiyo ya Old Trafford kusajili wachezaji. 
Amekuwa akisaka beki wa kushoto, kiungo na mshambuliaji Ulaya mzima.
Mlengwa mkuu: Manchester United inataka kumsajili mshambuliaji wa Atletico Madrid, Diego Costa
Flying high: Diego Costa and Atletico hit the top of La Liga after beating Malaga 1-0
Diego Costa aliiwezesha Atletico kupanda kileleni mwa La Liga baada ya kuifunga Malaga 1-0

Msaka vipaji mkuu wa United, Robbie Cooke alimshuhudia mchezaji wa bei ghali Costa akicheza dakika zote 90 huku Atletico Madrid ikishinda 1-0 dhidi ya Malaga Jumamosi.
Koke – mchezaji ambaye United wamekuwa wakihusishwa naye lakini hawana nia ya kumsajili mwezi huu – alifunga bao pekee kwenymchezo huo.
Cooke alikuwa mmoja wa watu wa benchi la Ufundi walioambatana na Moyes kutua Old Trafford wakitokea Everton na mpango huo ulimfanya asafiri kutoka pwani ya kusini ya Hispania hadi kaskazini mwa San Sebastian, kumuangalia mchezaji wa Atletico Bilbao, Herrara akicheza mechi ya kipigo cha 2-0 kwa Real Sociedad.
Costa, ambaye pia alitakiwa na Liverpool Agosti mwaka jana na hivi karibuni amekuwa akihusishwa na kuhamia Chelsea na Arsenal, amekuwa mmoja wa washambuliaji gumzo Ulaya msimu huu, baada ya kufunga mabao 19 katika mechi 18 na kuisaidia timu yake kuwa mpinzani mkuu wa Barcelona katika mbio za ubingwa wa La Liga.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 25 aliyekataa ofa ya uraia wa Hispania mwaka jana ili aichezee Brazil katika Kombe la Dunia, nchi yake halisi aliyozaliwa, alisaini Mkataba mpya na Atletico ili kumzuia kwenda Liverpool, lakini anaweza kuuzwa kwa Pauni Milioni 31.

No comments:

Post a Comment